Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mufindi tunao mpango wa kujenga Hospitali ya Halmashauri ili kupunguza tatizo kubwa la huduma ya hospitali, naiomba Serikali kusaidia katika ujenzi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali kumalizia kujenga kituo cha afya cha kata ya Mtwango, kata ya Mninga, kata ya Makungu na kata ya Mtambula. Wananchi pamoja na Mbunge tumejitahidi kujenga majengo katika kituo cha afya cha kata ya Mninga na kata ya Mtwango bado kumalizia. Pamoja na vifaa kama vile vitanda, blanketi, shuka na vifaa vingine ambavyo vipo kwa vituo vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuleta watumishi katika zahanati za Jimbo la Mufindi Kusini hasa katika zahanati ya Mbalamaziwa, kata ya Itandula, zahanati ya Ihowanza zahanati ya Kibao na zahanati ya Makungu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi kuleta gari la wagonjwa katika kituo cha afya cha kata ya Makungu, gari hii litahudumia kata ya Idete, kata ya Kiyowela na kata ya Makungu. Wananchi wa kata hizi wanapata shida sana hasa akina mama wakati wa kujifungua, wanashindwa kufika katika kituo cha afya sababu ya umbali, zaidi ya kilometa 60 mpaka 80 hadi kituo cha afya cha kampuni ya MPM. Naomba sana Serikali kutuletea ambulance kwa ajili ya wanachi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.