Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitoe shukrani kwa Serikali kwa kutenga fedha za ujenzi wa hospitali ya Mkoa wa Katavi. Mheshimiwa Waziri Mkoa wa Katavi ni eneo linalokuwa siku hadi siku na una changamoto kubwa za afya. Ni vema Serikali ikaweka kipaumbele kikubwa kujenga Hospitali ya Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Tanganyika haina Hospitali ya Wilaya, tunaomba Serikali kupitia Wizara ya Afya itupatie fedha za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kwani suala la huduma hiyo ni muhimu sana na ukizingatia jiografia ya Wilaya yangu ni ngumu sana na ndiyo Wilaya pekee yenye eneo kubwa sana kuliko Wilaya zote ambazo zipo Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Tanganyika ina vituo vitatu tu japo ni Wilaya kubwa na ina idadi kubwa ya watu, bado ndiyo eneo ambalo lina vituo vichache sana. Naiomba Serikali itupatie vituo vipya vya afya ambavyo vitarahisisha kutoa huduma ndani ya Wilaya, na kupunguza mzigo mkubwa kwa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado niiombe Wizara katika vituo tulivyonavyo ndani ya Wilaya vituo hivyo bado huduma hizo ni duni sana. Naomba kituo cha Karema, Mwese na Mishamo viboreshwe na viwe na hadhi. Ni matumaini yangu Serikali italiangalia kwa jicho la huruma kwa kuboresha vituo hivyo kwa kuvifanyia ukarabati na kupeleka dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ambulance, tunaomba ombi maalum la kupatiwa gari la wagonjwa, katika maeneo yenye uhitaji mkubwa ni Wilaya yangu ambayo ina taabu kubwa sana. Hivyo tunasisitiza ombi hili litiliwe mkazo mkubwa na muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani na ninaunga mkono hoja.