Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kama ifuatavyo:-

(i) Katika hospitali ya Wilaya ya Tunduru kuna tatizo la chumba cha kuhifadhi maiti cha kisasa na katika hospitali ile hamna wodi ya kulaza wagonjwa waliofanyiwa upasuaji, wagonjwa hao hulazwa katika wodi ya magojwa mchanganyiko kitu ambacho kina hatarisha afya ya wagonjwa hao.

(ii) Katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina kata 39 lakini kuna vituo ya afya vitano tu jambo ambalo linasababisha wananchi wanapata shida kutembea kilometa ndefu kufuata huduma za afya.

(iii) Katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna Hospitali ya Mission ya Mbesa ambayo inahudumia wananchi zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wa Tunduru na Wilaya jirani ya Namtumbo. Hospitali hii ina madaktari wanne tu, kati yao wawili ni wazungu ambao mkataba wao unaisha mwezi Juni, 2017. Hivyo naomba Serikali ipeleke madaktari kulingana na mkataba wa Serikali na hospitali hiyo.

(iv) Katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru tuna upungufu mkubwa wa wafanyakazi katika sekta ya afya. Zaidi ya wafanyakazi 700 wanahitajika ili kukidhi mahitaji ya zahanati zilizopo. Tunaomba sana ajira zitakapotangazwa tuangaliwe kwa jicho la huruma ili kututengea wafanyakazi katika sekta hii ili kunusuru wananchi wa Wilaya ya Tunduru.

(v) Kuna upungufu mkubwa wa dawa katika zahanati, vituo vya afya kwa ajili ya kuhudumia wananchi wetu, sambamba na upungufu wa vifaa tiba ikiwa ni pamoja na kukosekana kabisa kwa ambulance katika vituo vyetu vya afya ukizingatia Wilaya ya Tunduru ni eneo kubwa sana, wananchi wanatembea zaidi ya kilometa 100 kufuata Hospitali ya Wilaya, watu wanabebana kwenye matenga, akina mama wajawazito wanabebwa kwenye matenga kufuata huduma za afya.

(vi) Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi Hospitali ya Mission Mbesa kuwa Hospitali Teule kwa vile inahudumia wananchi wengi sana hasa wa hali ya chini wa Tunduru na Namtumbo. Ninaomba basi ahadi ile itekelezwe ili kupandisha hadhi hospitali ile kuwa Hospitali Teule kama ilivyoahidiwa na Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

(vii) Katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 tumeahidi kutoa posho kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 65, mpango huu utaanza lini ili kusaidia wazee hawa kupambana na hali ngumu ya maisha inayokabili wananchi?

(viii) Uboreshaji wa vituo vya afya katika kituo cha Mtina, Mchoteka, Nkade ili viweze kufanya upasuaji wa kawaida, mpaka leo vituo hivyo havina vyumba vya upasuaji, wananchi wanapata huduma hiyo Hospitali ya Mbesa au Hospitali ya Wilaya. Hivyo tunaomba tupatiwe vyumba vya upasuaji katika vituo vyetu vya afya na kuongeza vituo vingine vya afya kama tulivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.