Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Afya ni kigezo kimojawapo katika maisha ya mwanadamu. Hivyo basi, sekta ya afya ni muhimu sana katika mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ugonjwa wa UKIMWI kwa akina mama ambao wamejifungua salama, kumekuwa na uhaba wa dawa kwa akina mama wajawazito na waliojifungua salama. Mfano, mama mjamzito anachukua dawa hospitali ya Vwawa na anaishi Usangu. Baada ya kupata mtoto na mtoto kufikisha miaka miwili mama anatakiwa kurudi kituo chake cha kwanza ili kuendelea na dawa. Ikifika wakati wa kurudi hospitali ya awali mama anaacha kwenda kuchukua dawa kwa sababu mbalimbali. Kwa mfano, umbali wa vituo vya afya vya kuchukulia dawa, gharama za usafiri, majukumu ya malezi na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ya msingi kwa Wizara ni kwa nini Wizara isiweke mpango wa kutoa dawa kwenye ngazi ya zahanati zilizoko karibu na wananchi ili kuendelea kuokoa nguvukazi hii ya Taifa letu. Mfano, mtu anatoka Ichesa kwenda Hospitali ya Wilaya ya Vwawa kilometa 45 hadi 50, barabara ya vumbi na usafiri wa bodaboda. Hii inasabishia watumiaji wa dawa kuacha dawa na kuendelea kuwa na madhara yatokanayo na magonjwa nyemelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na changamoto za vifaa tiba kwenye hospitali zetu, bado wajawazito wanatakiwa kuwa na vifaa vya kujifungulia. Mfano gloves, code tie inayotumika kufunga kitovu cha mtoto anapozaliwa, pamba na gauze. Je, Waziri anatusaidiaje kwenye suala la vifaa hivi kwa wanawake wanaojifungua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa aina ya folic acid kwa wajawazito bado zimekuwa adimu sana kwenye hospitali zetu, badala ya kutolewa bure mama mjamzito analazimika kununua kwenye maduka ya dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nizungumzie kuhusiano na upungufu wa Madaktari Bingwa kwenye hospitali zetu za rufaa sambamba na wakalimani wanaotumia lugha za alama kwa walemavu wanaokwenda kutibiwa katika hospitali zetu.