Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja na napongeza jitihada zako ikiwemo upatikanaji wa dawa katika hospitali zetu. Niombe gari la wagojwa katika tarafa ya Matui ambayo ina population kubwa ya watu. Gari hilo likae kituo cha afya Engusero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba daktari wa Anesthesia katika kituo chetu Engusero ili operations ziweze kuendelea. Pia tunaomba madaktari na ma-nurse, Wilaya ina upungufu wa watumishi hao ikiwemo Daktari wa Kinywa na Meno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba ujenzi wa maabara ya Wilaya maana iliyopo ni chumba kidogo Prime Minister alikiona akashangaa na akaniambia nikuambie.

Mheshimiwa Waziri, tunaomba upanuzi wa kituo cha afya cha Sunya maana kinabeba wagonjwa zaidi ya 30,000 tunaomba maabara na upanuzi wa majengo (wodi).