Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upungufu wa dawa nchini; kumekuwa na upungufu wa muda mrefu wa dawa hapa nchini, tatizo hili limekuwa la kudumu na kwa kuwa chanzo kikubwa cha fedha kwa ajili ya kununua dawa inategemewa na mapato ya makusanyo ya kodi mbalimbali hapa nchini. Hata hivyo, kumekuwa na mifuko ambayo inaanzishwa na chanzo cha mapato kwa ajili ya mfuko huo unakuwa wa uhakika na kuleta ufanisi unaokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano ni Mfuko wa Barabara, Miradi ya REA ambayo chanzo cha mapato inatokana na fedha za mafuta na mfuko huo fedha zake haziguswi (ring fenced). Kwa kuwa dawa ni suala muhimu sana kwa ajili ya maisha ya Watanzania, hivyo ni wakati muafaka sasa Serikali ianzishe mfuko maalum wa dawa na fedha zake zitokane na chanzo cha uhakika ili kupunguza na kuondoa kabisa tatizo la ukosefu wa dawa hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Taifa ya Mount Meru; Hospitali hii ndiyo hospitali inayotegemewa katika Mkoa wa Arusha, hata hivyo kuna changamoto katika utoaji wa huduma kwa vifaa muhimu kama x-ray machine kuharibika mara kwa mara. Serikali ione umuhimu wa kuiwezesha kwa kiasi kikubwa hospitali hii ambayo ni muhimu kwa Mkoa wa Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni motisha kwa watumshi wa afya. Watumishi wa afya nchini ni kada muhimu sana ambayo wameamua kufanya kazi kubwa ya kutoa huduma kwa Watanzania wote. Hata hivyo, suala la afya ni muhimu sana kwa ustawi wa nchi yetu. Serikali lazima itazame kwa upya maslahi ya watumishi wa afya hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazee; kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya Serikali kuwa itaboresha makazi ya wazee, jambo hili limekuwa linaandikwa kwenye vitabu bila utekelezaji. Wazee ni hazina ya nchi, tunapaswa kuwaenzi na kuwahudumia. Serikali ijipange vizuri ili kuhakikisha makazi ya wazee yanaboreshwa.