Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atakapohitimisha hoja yake, atolee maelezo mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, gari la wagonjwa ambalo Wizara iliahidi kuwa imetenga shilingi milioni 20 katika mwaka wa fedha 2016/2017 katika Wilaya ya Muheza: Je, ni lini gari hilo la wagonjwa litafika Muheza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Mheshimiwa Waziri aliahidi kupeleka gari la wagonjwa katika Zahanati ya Mgambo, Amani itakapofika mwezi Januari, 2017 lakini sasa ni mwezi wa Tano hakuna utekelezaji. Wananchi wanapata usumbufu mkubwa katika upatikanaji wa dawa hasa wanaotumia bima kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa dawa katika hospitali zetu. Wizara imeandaa utaratibu gani kupitia MSD ili angalau kila penye Hospitali ya Wilaya kuwe na duka la dawa ambalo kadi ya bima inaweza kutumiwa na mgojwa kupata dawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamii ya mabohora Tanga wametoa mashine ya CT-Scan kwa Hospitali yetu ya Bombo, lakini inasemekana hakuna jengo special. Kama ni kweli, Serikali ina mpango gani kuharakisha ujenzi wa hilo jengo ili mashine zifungwe na kutumika?