Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Kakonko kwa muda mrefu imetumia Kituo cha Afya Kakonko kama Hospitali ya Wilaya. Naomba Wizara ya Afya isaidie kusukuma Halmashauri ya Wilaya na TAMISEMI kujenga Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Watumishi wa Afya Wilayani Kakonko ni mkubwa sana. Uhaba huo ni Madaktari wa kufanya kazi katika Vituo vitatu, yaani Kakonko, Nyanzige na Gwanumpu. Aidha, kuna uhaba wa kutoa huduma kama AMO, Core Nurses.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la akinamama kutozwa fedha wanapopeleka watoto clinic kupimwa. Hali hii inajitokeza kwa mama kuwalipa wahudumu wa afya (binafsi). Kwa nini kazi hiyo isifanywe zahanati?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Watendaji wa Ofisi ya Maendeleo ya Jamii watoe elimu ya ujasiriamali kwa wananchi ili waanzishe vikundi vya kujitafutia kipato. Aidha, hamasa itolewe kwa wananchi kusajili vikundi kama VICOBA, SACCOS na vikundi vinginevyo vya kijasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba matibabu bure ya wazee kutolewa kama Sera ya Wazee inavyoeleza. Wazee walipwe pensheni kila mwezi kama ilivyowahi kuamuriwa na Bunge. Vile vile Vitambulisho vya Wazee vitolewe kwa muda muafaka, kwani Mheshimiwa Waziri aliagiza viwe vinatolewa kabla ya tarehe 30/12/2016, lakini hadi sasa Wilaya ya Kakonko wazee hawajapata vitambulisho, sambamba na sensa ya kuwatambua wazee wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ifanyiwe marekebisho ili kuepuka watoto (underage) kuolewa kwa kigezo cha umri wa kuolewa. Pia watoto wa kike wanaobeba mimba shuleni wapewe nafasi ya kuendelea na masomo. Wizara ishauriane na Wizara ya Elimu kuweka Sera (re-entry policy) ya wanaobeba mimba kuendelea na masomo mara baada ya kujifungua. Hii itasababisha watoto hawa kupata haki ya elimu.