Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mchango wangu wa maandishi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika michango ya Waheshimiwa Wabunge katika Wizara hii, wameeleza tatizo kubwa la ukosefu wa X-Ray katika Hospitali zetu. Katika Jimbo langu ambalo lina Hospitali moja ya Shirika la Dini, hatuna huduma ya X-Ray. Jitihada nyingi zimefanyika zikiwemo pamoja na mchango wa Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kuchangia Shilingi milioni 40 mwaka 2010. Nasi Halmashauri kwa upande wetu katika Bajeti ya mwaka huu wa fedha 2017/2018, tumetenga Tanzania Shilingi milioni 20. Hivyo tunaomba Wizara itusaidie kuwasiliana na wenzetu wa Bima ya Afya ili waweze kutukopesha kifaa tiba hicho, kwani tayari tunazo shilingi milioni 60 mkononi ambazo zitaweza kuwashawishi wenzetu kutukopesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 127 inaonesha hali ya Halmashauri. Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa hali yake ya upatikanaji ni asilimia 77. Ukilinganisha na Halmashauri nyingine, Halmashauri hii ni miongoni mwa Halmashauri chache ambazo upatikanaji wake wa dawa bado uko chini. Naomba Mheshimiwa Waziri atakapohitimisha, atuambie ni kwa nini Kilwa? Je, kuna mikakati gani ya kutatua tatizo hili ili kuhakikisha tunapata dawa kama zinavyopata Halmashauri nyingine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) inaonesha zaidi ya Tanzania Shilingi bilioni nne zimepotea kutokana na miradi iliyokamilika lakini haifanyi kazi. Katika Jimbo langu la Kilwa Kaskazini, kuna zahanati sita ambazo majengo yake yameshakamilika, lakini bado hazijafunguliwa. Ni Zahanati ya Hongwe, Mpindimbi, Nambondo, Miyumbu, Marendego na Mwengei. Naomba kwa usimamizi wa Serikali izifungue zahanati hizi kwani nguvu za wananchi na Serikali zimepotea bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, katika sakata la vyeti feki, uhakiki wa vyeti, Wilaya yangu imeathirika sana hasa katika Hospitali ya Wilaya ya Kinyonga na Hospitali ya Kipatimu. Madaktari tegemezi wamekumbwa na tatizo hilo. Naomba watakapopanga mgawanyo wa Madaktari kutokana na tatizo hili, Wilaya yangu iangaliwe kwa jicho la huruma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.