Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kutoa kipaumbele kwa Wizara ya Afya. Hivyo basi, pongezi pia ziende kwa Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile pongezi nyingi kwa Waziri husika Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Naibu wake Dkt. Hamis Kigwangalla na Watendaji wote, kwa kusimamia vyema Wizara hii na matunda tunayaona, pamoja na ufinyu wa bajeti. Waswahili husema, ng’ombe haelemewi na nunduye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali ipandishe hadhi baadhi ya Vituo vya Afya vilivyopo Mkoa wa Pwani. Hii ni kutokana na umuhimu wa kuongeza/kupanua huduma kwa jamii. Vituo hivyo ni Kibiti, Muhoro (Rufiji), Mlandizi (Kibaha Vijijini), Ubena (Chalinze), Mzenga (Kisarawe) na Kibaha Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwa kutaimarisha huduma hizo, pia vituo hivi viko barabara kuu za mkoa ambapo usafiri wa aina mbalimbali hupita hivyo, endapo kukitokea ajali kunakuwa hakuna uwezo wa kutoa huduma na hivyo kulazimika kusafiri kwenye Hospitali za Wilaya au kupelekwa Hospitali za Mkoa jirani, Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chonde chonde, pamoja na matatizo ya kiufundi (kama yapo) tusaidiwe X-Ray ya Mafia ipate ufumbuzi wa kufungiwa, ukizingatia Mafia ni kisiwa na hawana pa kukimbilia endapo imetokea dharura. Nimalizie kwa kuomba suala la maji kwa zahanati na vituo vya afya. Ni muhimu, kuwe na elimu ya uvunaji maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.