Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ASHA M. JECHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Naipongeza Wizara kupitia Mheshimiwa Waziri, Naibu, Katibu Mkuu pamoja na Watendaji wote kwa juhudi kubwa wanazofanya kushughulika na afya za Watanzania na kuboresha maendeleo ya jamii. Sambamba na hilo ni weledi wao ulioifanya Wizara hii kusonga mbele na kuleta mabadiliko makubwa ya kiutendaji na kuwahudumia Watanzania popote walipo mjini na vijijini. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwezeshaji wanawake kiuchumi. Naipongeza Wizara kwa mipango mizuri ya kuwainua wanawake kiuchumi. Hata hivyo, bado juhudi zaidi zinatakiwa kuchukuliwa kwani bado wapo wanawake wengi wajasiriamali hawajawezeshwa kiuchumi, wanajitahidi wenyewe lakini kutokana na mtaji kuwa mdogo wanashindwa kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki ya wanawake, iko mbali na wanawake walioko vijijini. Je, ni lini Wizara itaielekeza benki hiyo kufungua angalau dirisha katika maeneo ya vijijini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hisa katika Benki ya Wanawake, wapo baadhi ya Wabunge tumeshiriki kununua hisa kwa ajili ya uanzishwaji wa benki hii. Je, ni lini tutaarifiwa juu ya kinachoendelea na hatma yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea kuhusu unyanyasaji wa wanawake na watoto. Naipongeza Serikali kwa juhudi mbalimbali inazochukua katika kukabiliana na tatizo hili lakini bado juhudi zaidi zinahitajika kwa kuungana pamoja kupiga vita hali hii isiendelee. Wazee/wazazi waache tabia ya kuwatumia watoto wadogo kama kitega uchumi kwa kuwaingiza katika ajira za watoto hasa kuwatumikisha majumbani na kuwakosesha haki zao za elimu na matunzo ya karibu ya wazazi. Kwa nini Wizara isielekeze ajira za majumbani zifanywe na watu wazima badala ya kuwatumia watoto wadogo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii, ahsante.