Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi nichangie kwa uchache tu, kuhusu Wizara hii ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mwenyezi Mungu Subhana wataala kwa kunipa afya njema na kusimama leo mbele ya Bunge lako Tukufu ili niweze kuchangia machache kwa lengo la kuisaidia Serikali kuboresha pale ambapo naamini inaweza kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoifanya. Mimi simpongezi tu Mheshimiwa Rais hivi hivi bali nampongeza kwa kuzingatia vigezo vitatu vya leadership. Kwanza ujasiri, pili, uthubutu na tatu kujiamini kwake. Katika falsafa za kiongozi bora akiwa na misingi hii mitatu, anakuwa kiongozi bora. Ndivyo ambavyo Mheshimiwa Rais anafanya, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wake pamoja na Serikali yote kwa ujumla. Nampongeza sana Mheshimiwa Harrison Mwakyembe, Naibu wake na Watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kweli Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18 na hata Sera ya habari ya 1993 inazungumza juu ya kwamba kila mtu ana haki ya kupata habari. Sina haja ya kwenda mbali sana, lakini haki ya kupata habari pamoja na wajibu wa kupata habari vyote hivi vinategemeana. Haki bila wajibu haiwezi kwenda. Si kwa sababu tu Katiba inatamka na Tanzania imeridhia matamko ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika, watu wavunje sheria tu kwa makusudi kwa sababu Katiba imetaka hivyo. Sidhani kama hiyo ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti Waadishi wa habari wa nchi hii wanafanyakazi kubwa sana. Vyombo vya habari vinavyafanya kazi kubwa sana, lakini kuna kitu kimoja ambacho sisi waandishi tunasahau. Mwandishi wa habari ni sub-soldier, hili lazima ulielewe. Hakuna nchi yoyote duniani, mimi siamini na sijawahi kuona kwamba vyombo vya habari vinaweza vikaamka tu magazeti yanatunaka tu watu wakaa kimya. Ndiyo maana ya kuwa na state. State maana yake ni ku- protect citizen wake katika Taifa lile. Ndivyo ambavyo kazi inafanya. Nawashukuruni sana Mheshimiwa Waziri endeleana na moyo huo huo, chapa kazi tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nizungumzie kidogo kuhusu michezo. Mpira wa miguu ndio mchezo unaopendwa kuliko yote duniani kwa sasa hivi. Naipongeza sana timu yetu ya Serengeti boys na viongozi wa TFF. Hata hivyo, timu za vijana hazijengwi na TFF, zinajengwa na vilabu. Hili lazima TFF; na nashukuru rais wa TFF, Rais anayemaliza muda wake yuko hapa; ninachosema lazima Vilabu viakikishiwe kwamba kweli vina wachezaji wa timu za vijana. Tusijidanganye tukasema TFF ama Serikali inaweza kuwa na academy yake kuwatengeneza wachezaji, hiyo haijatokea duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti ni imani yangu kwamba Mheshimiwa Waziri na bahati nzuri sasa kwamba FIFA imetoa room kwa Serikali ku-interfere pale ambapo wanaona mashirikisho ya mpira na michezo mingine hayafanyi vizuri tofauti na ilivyokuwa wakati wa Blatter. Kwa hiyo Mheshimiwa Mwakyembe you have the room, ukiona hapaendi vizuri FIFA imetoa hiyo. Jitahidi sana, lazima tuhakikishe vilabu hivi vinakuwa na timu za vijana zilizo imara ili tupate national timu inayoweza kwenda kushindana. Otherwise tutapiga kelele miaka nenda, miaka rudi, hatuwezi kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nidhamu pia kwa wachezaji, wachezaji wasipokuwa na nidhamu; hata hapa ndani ya Bunge ndiyo maana tunatunga hizi kanuni ili tuwe na nidhamu. Kama hawana nidhamu hatuwezi kufanya vizuri katika michezo, hili lazima tuliangalie. Sitaki kuzungumzia rafiki zangu hapa wananiambia point za Kagera nasema hizo nawachia TFF watajua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kidogo kuhusu Shirika la Utangazaji Tanzania. Mimi kwa maono yangu na kwa mtazamo wangu na kwa analysis nzuri tu kwamba uanzishwaji wa Redio Tanzania kubadilishwa kuwa Shirika la TBC lazima kuna makosa yalifanyika. Hili shirika ni shirika la habari, lakini halina tofauti kimuundo na TANESCO, halina tofauti kimuundo na bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo TBC pale kuna Wakurugenzi zaidi ya 10, mameneja 14 wakati pale wanahitajika viongozi wanne tu. Mkurugenzi Mkuu, Mkuu wa vipindi, CP, Meneja wa Ufundi, umemaliza. Mheshimiwa Waziri angalieni Muundo wa lile Shirika ndiyo maana leo wanapata tabu sana. Lile ni broadcasting house siyo Shirika la Uzalishaji, hapo ndipo tatizo linapotokea. Leo Ryoba anapata tabu sana pale kwa sababu anashindwa kuendesha lile shirika limekuwa ni kama shirika la uzalishaji na si broadcasting house. Angalieni hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna matatizo ya vifaa, hata ile studio ambayo ilitengenezwa wakati ule wa TVT ndiyo studio inahusika kuzalisha matangazo yaende huko nje. Usikivu umekuwa duni. Leo ukienda huko Pangani wapi unasikia KBC Kenya. Hapa Chemba ukienda kwa Mtoro ndiyo hatusikiki kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko Mlalo ndio kabisa wanasikia Kenya. Ukienda huko Tanganyika huko wanasikiliza Kongo. Lazima tufanye investment ya kutosha. Hata live coverage ni aibu kabisa kwa Shirika kubwa kama lile kwenda kuazima chombo cha kurushia matangazo kutoka kwa mtu binafsi. Kabisa! Ni aibu! Juzi Rais anakwenda Mtwara wameazima chombo kwa mtu binafsi Benjamin, pale wanalipa sijui dola mia sita sijui ngapi ni aibu. Msaidieni Ryoba yule, vinginevyo atashindwa. (Makafi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hii tunayotumia hapa Bunge imetengenezwa tu amplifier lakini pia zile flyways zina life Span. Nunueni vingine na nimefurahi kusikia Mheshimiwa Waziri kwamba mwezi wa sita vitakuja vingine. Wazee sisi wengine tumekulia pale kama siyo TBC tusingekuwa hapa. Mimi mtoto wa mfinyanga vyungu naingia Bungeni, kama si TBC tusingekuwa hapa leo. Kwa hiyo, isaidieni sana TBC hasa kwenye vifaa lakini na muundo wake. Mheshimiwa Mwakyembe nakujua fanyakazi yako angalia ile shirika vizuri badilisha style irudi kuwa broadcasting house na siyo shirika la uzalishaji. Weka viongozi wanne tu Mkurugenzi Mkuu, wa Ufundi, Control programs umemaliza unasonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja. Ahsante sana.