Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi niungane na wenzangu wote kumpongeza Waziri na timu yake kwa kazi nzuri japo tuna maeneo ya kushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza, mwezi Februari sikumbuki tarehe nilikuwa na swali hapa kwa Wizara hii kuhusiana na kumomonyoka kwa matumizi ya lugha ya kiswahili ambako kwa kweli kunakithiri na pia hali ya kuchanganya lugha. Imefikia hatua hivi sasa kwenye vyombo vya habari msanii ama mtu yeyote ameitwa pale anazungumza Watanzania wote wanasikiliza, watoto wanaojifunza afadhali sisi tayari tulishapa misingi, unasikia anasema nyimbo hii niliitunga mwaka jana, mwingine anasema, tena watangazaji wa soka wale, kwa mfano anasema timu ya Lipuli imetoka sare na timu ya Polisi kwa hiyo wameshindwa kupata matokeo. Wakati tunafahamu kwamba matokeo ni ama kushinda ama kushindwa ama kutoka sare.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuna maudhui yanabadilishwa ambayo kwa kiwango kikubwa kwa hawa watoto ambao wanakua sasa tunashindwa kujua tunawafundisha hii version mpya ya kiswahili ama tunaendelea na ile ya kwetu? Wakati huo huo Waziri kwenye ukurasa wa 25 anaongelea kiswahili kuwa bidhaa, ukurasa mwingine sikumbuki anasema ni lugha ya kumi katika lugha 6,000, hizo zote ni sifa ambazo zitakamilika endapo tutakuwa na jitihada za dhati za kutunza kiswahili.

Nafahamu kwamba kwenye kukua kwa kiswahili katika maeneno mapya yanayokuja nayo ni sehemu ya kukuza lakini iwe guided. Naamini kuna wataalamu wetu ambao wanaweza kutuongoza ili hata sisi ambao walau tunajua kile tulichofundishwa miaka hiyo tufahamishwe rasmi sasa kwamba imebadilishwa siku hizi ni nyimbo hii sio wimbo huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri wakati ananijibu mwezi Februari alisema kuna sera inakuja nikafurahi sana. Nilitarajia hotuba hii isheheni hiyo mikakati ya sera na iongelee kwa uzito kwa sababu hili jambo linakera.

Tunaomba tuzungumze kiswahili fasaha ili hiyo habari kwamba ni bidhaa, ni lugha ya kumi kweli iwe na tija vinginevyo tutaishia kuiandika tu hapa, hiyo moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, siku moja nilihudhuria mechi ya soka ya Simba na nafikiri ni Polisi Morogoro ilikuwa mwaka jana au mwaka juzi sikumbuki vizuri na mabadiliko hayajafanyika. Lile gori la uwanja wa Jamhuri Morogoro upande wa Polisi nafikiri ni Kaskazini, goalkeeper akidondoka kuna shimo pale unaweza usimuone tena refa anaweza akamtafuta. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hapo ndipo tunatoa klabu bingwa ya Tanzania ikacheze na National Al-Ahly, tunajidanganya. Core function ya soka ni pale kwenye pitch. Tunazungumza habari ya corporate, ni sawa lakini business kubwa kabisa ya soka ni kwenye pitch. Hivi kwa nini msikae na hizo corporate tukatafuta namna ambavyo kila timu inavyopanda daraja tunaweka mkakati wa pamoja wa kibiashara na kijamii tunapata uwanja, pitch ile hata kama hakuna jukwaa. Huwezi kutoa klabu bingwa kwenye uwanja ule wa Morogoro ambao goalkeeper akidondoka humuoni ikaenda kucheza na National Al-Ahly au Zamalek, haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nampongeza sana Ndugu yetu Malinzi kwa mambo anayoyafanya, anafanya mazuri tu lakini yako ya msingi. Kwa mfano, amezuia hapa juzi, kuna watu walitaka kuleta fujo, mpira unachezwa uwanjani, ukishindikana mezani, ukishindikana maandamano, haiwezekani! Acha watu wacheze mpira uwanjani, wewe simamia, lakini Malinzi rudi kwenye core function mpira unachezwa kwenye pitch tukose majukwaa lakini pale tucheze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kwenye hotuba sikumbuki ukurasa wa ngapi kuna vituo 56 vitaanza vya kukuza soka la watoto, tuondokane na hii Dar es Salaam, Mwanza na Arusha syndrome. Kuna wachezaji wa mpira kutoka maeneo mengine kwa mfano Biharamulo kuna vipaji.

Waziri atuhakikishie namna gani ata-distribute tupate kituo Biharamulo, Mtwara na sehemu nyingine habari ya Dar es Salaam, Arusha achana nayo, vipaji vipo vijijini. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakuja kwenye suala la sanaa, nimesoma ukurasa fulani hapa unasema kwenye kukuza sanaa lilifanyika kongamano/warsha Kisarawe kwenye shule moja. Jamani lazima tuangalie coverage, tukisema hili ni tukio moja Kisarawe halitatusaidia kuna mambo hayahitaji hata bajeti. Hivi tukihakikisha kwenye curriculum ya shule ya msingi kuna siku moja kwa wiki au kila baada ya wiki mbili, mwalimu mmoja ametengenezwa vizuri anawaandaa watoto wanacheza ngoma za kienyeji, anafanya tathmini, anawaelekeza, hakuna bajeti ni wale wale. Kwa hiyo, tutafute coverage kubwa siyo lazima kila wakati bajeti ni pesa kuna bajeti ya muda tu na bajeti ya kuandaa walimu kule chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, habari ya soka, pia kuna habari ya UMISETA. Wakati huo UMISETA ilikuwa inatengeneza watu kwa sababu nguvu kubwa ilikuwa inawekwa sasa hivi tunaisikia UMISETA passively yaani unaisikia juu juu tu. Ndiyo maana hata hawa akina Samatta wanatokea kwa ajali tu, hata hawa Serengeti Boys kama alivyosema msemaji mmoja aliyetangulia ni ajali. Kuna hatari ikawa wanatoka huko amepata sifa kubwa TFF kazi wameifanya, lakini baada ya hapo hutaona jambo lingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumalizia kwa habari ya kwenye ligi kuu ya soka kama alivyosema msemaji mmoja aliyetangulia. Tutafute namna gani ya kulinda vipaji vyetu, wazo limetolewa hapo, tuhakikishe kwa mfano kwenye first eleven katika dakika zote tisini kuna walau under twenty wa Tanzania kwenye kila mechi inayochezwa ya Ligi ya Vodacom. Amesema Mbunge mmoja hapa naomba kusisitiza, hiyo ndiyo namna ya kulinda. Pia tutafute namna ambavyo hata wale wachezaji saba waliosajiliwa kutoka nje ya nchi tuwalete ili watuongeze nguvu ligi yetu iwe na mvuto zaidi, lakini sio lazima wote watano wawe kwenye mechi moja, uwa-limit kwamba wale wageni kuna limit fulani ili wa ndani nao wapate fursa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, mchango wangu ni huo.