Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

HE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Habari na Michezo ni Wizara muhimu zaidi ikilenga kuinua michezo, burudani na kuelimisha jamii kupitia nyimbo na michezo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nahitaji kujua ni lini Serikali itakamilisha kuweka ofisi za usajili kila wilaya ofisi za COSOTA na BASATA ili kuondoa usumbufu kwa wasanii wakitaka kusajili kazi zao mpaka waje Dar es Salaam; huoni kama huo ni usumbufu kwa wadau wa sanaa. Je, hamuoni kama huu ni upotevu wa kodi kwa sababu msanii mchanga hawezi kujigharamia mpaka afike Dar es Salaam na pia kuna urasimu mkubwa katika ushuru wa stamp? Je, ni lini Serikali itaondoa kero hizi; itapunguza urasimu kupitia usajili COSOTA, BASATA na TRA, wasanii kuibiwa kazi zao, kujenga ofisi kila Wilaya, kuzingatia maadili katika kazi za sanaa za maigizo, michezo, nyimbo, vichekesho vinavyokiuka maadili ya Kitanzania? Ni lini Serikali kupitia COSOTA/BASATA itaacha ubaguzi kwa kuwafungia nyimbo/maigizo kazi za sanaa kwa baadhi ya watu na wengine hawachukuliwi hatua wanapotengeneza video zinazochefua jamii. Itawatafutia masoko wasanii. Kazi za sanaa zinalala ukizingatia nchi kama Kenya wako vizuri.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Bunge kuonesha live. Ni lini Serikali italiachia Bunge kuoneshwa live. Je, hamuoni kwamba kuzima Bunge mnajichimbia kaburi nyie wenyewe. Mmeondoa uhuru wa Watanzania kuongea kwa uhuru, kuonya, kuelimisha na kuikumbusha Serikali kupitia Bunge live na Serikali yao.

Mheshimiwa Spika, Sheria kandamizi za mitandao. Hamuoni kwamba Watanzania pamoja na Sheria hii mpya ya habari hawajajifunza na kutambua vizuri matokeo yake. Mnawafungulia mashtaka Wapinzani tu CHADEMA, CUF wao CCM hawavunji Sheria? Acheni tabia ya kunyanyasa watu. Roma Mkatoliki mlimteka kwa sababu tu kaongea ukweli kaisema Serikali, Je, uhuru wa habari uko wapi?

Mheshimiwa Spika, habari Bunge; leo hata waandishi wa habari wanaoingia Bungeni hawapati taarifa kamili ili ziruke kwa Watanzania mpaka ziwe zimekuwa edited (filter) kitu ambacho kinapunguza ukweli wa habari. Wizara iangalie hili ili kuweka uhuru wa waandishi wa habari kupata taarifa kutoka Bunge.

Mheshimiwa Spika, kuchunga hotuba za Kambi Rasmi ya Upinzani. Hii ni kero na hailisaidii Taifa. Kambi ya Upinzani ni mbadala wa Serikali tawala katika kuisaidia Serikali kibajeti katika vipaumbele ili Wizara zisonge mbele. Sasa hotuba zinapofanyiwa editing, je, hamuoni kama mnapoteza lengo la Upinzani kuisaidia Serikali. Tunajenga nyumba moja na Taifa moja, ubaguzi usifanyike kwa Upinzani tu bali angalieni haki.