Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, TBC. Televisheni ya Taifa haifanyi matangazo kwa usawa hasa inapochukua matangazo ya kisiasa kwa uwiano sawa na vyama vingine. Pia TBC ijikite kutoa elimu ya uraia na mendeleo zaidi katika vipindi vyake badala ya kuweka vipindi vya muziki kwa muda mrefu zaidi.

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee viwanja vya michezo mikoani. Katika Mkoa wetu wa Mbeya hatuna viwanja vya kutosha vya michezo vinavyoweza kusaidia watoto wetu kujifunza michezo na kukuza vipaji kama mjuavyo Mbeya na viunga vyake bado vinatoa wachezaji bora wa michezo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, niongelee viwanja vya wazi. Viwanja vingi vimetaifishwa na watu wachache bila kuchukuliwa hatua za kisheria na kurudisha viwanja hivyo kwa wahusika ikiwemo Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, vazi la Taifa. Ni lini vazi la Taifa litakuwa tayari katika utekelezaji wa utumiaji huo. Kama Taifa tunahitaji utambulisho wa vazi letu.

Mheshimiwa Spika, sasa niongelee kuhusu timu ya mpira wa miguu. Tumekuwa jamii na Taifa la kushindwa kila wakati kwa Wizara kutowekeza zaidi katika timu hii, lakini Wizara kutosimamia miundombinu/aina ya namna ya kupata wachezaji bora toka sehemu mbalimbali ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, mwisho niongelee suala la ufungiaji wa wanamuziki. Siku za hivi karibuni Serikali imekuwa inawafungia waimbaji wa nyimbo za bongo fleva kwa kile kinachodhaniwa hakiwafurahishi watawala. Hii inaondoa ubunifu na hali ya wasanii kuimba hisia zao kwa usahihi. Serikali itumie ofizi zake kama BASATA kuwasimamia wasanii hawa kufuata kanuni na haki za wasanii bila kubagua na kupendelea kwa kutumia hisia za kisiasa tu.