Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza Waziri pamoja na timu yake yote kwa kuwasilisha vizuri hotuba yake nzuri iliyojaa matumaini ya kuinua Wizara hii katika Habari, Sanaa na Michezo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Serikali yangu tukufu kuwekeza katika suala zima la michezo wala isichukulie mzaha kwani sekta hii ikisimamiwa vizuri itakuwa inaingiza mapato mengi katika Taifa letu pamoja na kutangaza utalii katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Lushoto, Radio ya Taifa haipatikani kabisa zaidi ya wananchi kusikiliza Radio za Kenya. Hivyo, naishauri Serikali yangu tukufu ijenge minara ya redio katika Wilaya ya Lushoto kwani wananchi wanakosa taarifa muhimu pamoja na mawasiliano muhimu ya kuhusu nchi yao pamoja na nchi za nje.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Lushoto kuna vijana wengi wana vipaji vya sanaa na michezo lakini vijana hawa wameachwa huko vijijini na kupoteza vipaji vyao. Kwa hiyo, naiomba Serikali hasa Wizara ya Michezo itoe timu kwa ajili ya kwenda vijijini ili kwenda kuibua na kuwanusuru vijana ambao wana vipaji na kuwajengea uwezo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, Lushoto ni Wilaya kubwa ambayo ina vijana zaidi ya 250,000, lakini ndani ya Wilaya hakuna uwanja hata mmoja wa michezo. Kwa hiyo, naiomba Serikali ijenge uwanja wa michezo Lushoto Mjini. Pamoja na hayo, kujengwe Chuo cha sanaa katika Jimbo la Lushoto ili kuendeleza vipaji hivi vya vijana wetu hawa wa Kitanzania. Niishauri Serikali ifundishe michezo mashuleni pamoja na kupewa vifaa vya michezo katika shule zote.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali yangu tukufu kwa wale wote ambao wapo vijijini, wanamichezo pamoja na wasanii Serikali iwasaidie ili waweze kukuza vipaji vyao sambamba na kuwa na ajira kupitia kazi yao hiyo kwani wasanii wa vijijini wanapata tabu sana mwisho wa siku wanakata tamaa na kuiona Serikali yao haiwajali.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.