Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Bahati Ali Abeid

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. BAHATI ALI ABEID: Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri, Naibu Waziri na watendaji wa Wizara hii kwa kazi kubwa wanazozifanya. Mheshimiwa Waziri mna kazi kubwa ya kusimamia Taifa letu kuhakikisha mnajitahidi sana ili mila na desturi za nchi yetu na utamaduni wetu uendelee kubaki. Nasema hivi kwa kuona vijana wetu wanajiajiri kwa kuanzisha sanaa ya muziki huu wa kizazi kipya ambao baadhi yao hasa vijana wa kike huwa wanacheza wakiwa wana nguo ya ndani tu.

Mheshimiwa Spika, hivi Baraza la Sanaa la Taifa linaangalia maudhui ya nyimbo tu kama maneno yaliyotumika siyo au linawangalia kundi lote hata wachezaji? Kwani vijana wa kike baadhi yao wanatutia aibu sana. Mheshimiwa Waziri Wanawake tunadhalilika sana wakati mwingine unashindwa kuangalia TV ukiwa na watoto wako wa kiume kuogopa itatokea hiyo nyimbo yenye vijana waliovaa vibaya, Watanzania sio Wazungu hata kama tunataka muziki ukue siyo hivi. Namwomba Waziri akemee vikali kwani mila na desturi za Watanzania ni hazina kubwa aliyotupa Mwenyezi Mungu, tusiwaachie watu watuharibie.

Mheshimiwa Spika, michezo ni jambo ambalo linalitangaza Taifa letu na Tanzania, kwa kweli tunajitahidi ila viwanja vya michezo Tanzania Bara ni kidogo. Ni muhimu kila vinapopimwa viwanja tukumbuke viwanja vya mpira kwani vipaji vya michezo vinaanzia vijijini Wizara ikishirikiana na Wizara ya Ardhi jambo la kutengwa viwanja vya michezo linawezekana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.