Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Spika, habari; TBC mitambo iboreshwe, kuwa na uwezo wa kusikika nchi nzima hasa redio ambayo ni ya Taifa lakini haisikiki nchi nzima hasa wilaya na mikoa ya pembezoni kama Mkoa wa Kigoma na Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Spika, TBC (TV) mitambo yake ni chakavu iboreshwe. Vyombo vya habari kutokuwa huru; uwepo uhuru wa vyombo vya habari kama redio TV, Magazeti na kadhalika. Kuna fununu kuwa Serikali ina mpango wa kuzuia TV na redio kusoma magazeti asubuhi kwa Watanzania (yaani tuongee magazeti). Hii itazuia Watanzania wengi sana kukosa hata ile haki ya kujua nini kiko kwenye magazeti hasa kule ambako magazeti hayafiki kama Kakonko.

Mheshimiwa Spika, mitambo ya redio Kakonko/ Kibondo kutojengwa wakati bajeti ya 2016/2017 ilipitisha bajeti ya kujenga TBC redio boster. Mitambo hiyo haijajengwa hadi sasa.

Mheshimiwa Spika, michezo; tuandae michezo kuanzia shule za msingi/awali, sekondari, vyuo, na kadhalika. Hii itatengeneza “Pool” ya wachezaji watakaounda timu za kitaifa. Serikali itenge bajeti ya michezo hasa mpira wa miguu ili timu za kitaifa kama Serengeti boys zinapofanya vizuri ziweze kupewa fedha.

Mheshimiwa Spika, sanaa; chuo cha sanaa Bagamoyo kipewe fedha za kutosha ili kujiendesha na kiboreshe miundombinu yake kama studio ya kisasa. Serikali ilinde haki za wasanii pamoja na kupewa haki miliki lakini kazi zao bado zinaibiwa.