Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa ruhusa hii nami kuchangia Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi, inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Nichangie kwenye kituo changu cha Bububu.Kituo cha Bububu hakina Kompyuta, hakina photocopy machine, copy wanakwenda kutoa nje ya kituo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu matundu ya choo. Matundu ya choo hali ni mbaya katika kituo changu cha Bububu. Askari wanawake wanatoka nje wanakwenda kujisaidia na wao hawako salama, kwa sababu tunaijua Bububu ilivyo ni hatari. Tunamwomba Waziri kile kituo akitendee haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la watani zangu. Kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya, katika Jimbo langu kulikuwa na uhalifu mkubwa sana, amejitahidi uhalifu ule umepungua kwa asilimia mia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi kule sasa hivi wameanza kujikusanya vikundi wakiwa wanazungumza tunaita Zanzibar drip, wanasema uchaguzi upo kesho Maalim Seif anapewa nchi kesho. Tena niwahakikishieni kama ni uchaguzi umemalizika na tusubiri mwaka 2020, baada ya miezi mitatu, minne tutakuwa na wagonjwa wa hali nyingi, wagonjwa wa wasiwasi na wagonjwa wa presha kwa sababu akikaa tu Maalim Seif kesho anapewa nchi. Uchaguzi umemalizika tufanyeni kazi kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye kituo changu cha Polisi Bububu. Mheshimiwa
Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri alijitahidi sana kwa sababu pale palikuwa na Mwekezaji, wameondoka na kituo kipo salama kwa sababu sisi wenyewe wananchi tulikuwa hatuko salama kwenye kituo kile. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Naibu Waziri kwa hali aliyoichukua pale kwenye kituo akamwondoa yule mwekezaji na sasa hayupo, nashukuru kituo kimebakia salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia juu ya mia.