Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na vilevile nimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dakika zangu ndogo kwa hiyo siwezi kusema mlolongo mkubwa. Naipongeza hotuba hii ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Pia niwapongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake kwa hotuba hii ambayo ni nzuri, aliyoipanga na haina mjadala, isipokuwa kuna mambo tu madogo madogo yaweze kuwekwa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha Polisi Daraja ‘B’ Mkokotoni Unguja kina asilimia 60 na haya ninayozungumza yamo katika hotuba hii. Kituo hiki kina asilimia 60 Mkokotoni tayari kimeshakuwa kimefanikisha, lakini kuna vituo humu nchini ambavyo havina hadhi na havina mashiko. Tukizingatia katika Mkoa wangu wa Kusini Unguja kituo hiki cha Paje ambaye hapa kidogo mwenye hili Jimbo alilizungumzia lakini hakulitoa sahihi sana. Kituo kile hakina hadhi na ukipita pale utahisi kama hiki siyo kituo cha Polisi, kama wenyewe watakuwa hawapo pale nje basi huwezi hudhani kwamba hiki ni kituo cha Polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo pia hiki kilikuwa kimo ndani ya mgao kwamba kitengenezwe na kiwe kituo cha hadhi cha Wilaya ya Kusini, naomba kama hili suala kweli lipo basi hiki kituo kiweze kutengenezwa kwa sababu ukanda mzima ule ni ukanda wa watalii na watalii wote waliopo kile kituo hiki ndicho kinachohusika kuanzia Jambiani hadi Michamvi. Naomba kituo hiki kitengenezwe kuwa kituo cha hadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja. Ahsante sana.