Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza, napenda kuwapa pole wananchi wangu wote wa Dar es Salaam waliopata adha za mvua. Wengi wamepata mafuriko na nyumba zao hazikaliki, nawapa pole sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuchangia Wizara hii ya Maji. Kwanza niseme maji ni kilio. Maji ni mateso kwa mwanamke, mtoto na baba wa Kitanzania. Kwa kukosa maji kwa kweli wanapata mateso makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hivyo ndivyo kwanza niuongelee Mfuko wa Maji. Mfuko huu wa Maji naona ndiyo pekee ambao unatakiwa kutukomboa kwa kuona kwamba bajeti ya maji sasa inafeli. Mfuko huu wa Maji mpaka sasa unachangiwa kwenye mafuta Sh.50 tu, ningeomba uongezwe hiyo Sh.50 nyingine au ikionekana kwenye mafuta kunaleta inflation basi iongezwe kwenye pombe au tuangalie kwenye Mfuko wa Barabara kama tunaweza kutoa asilimia 10 iongezwe kwenye huu Mfuko wa Maji. Maana inavyoonekana theonly solution ya kumsaidia Mtanzania sasa hivi ni huu Mfuko wa Maji ambao ndiyo unaweza kusaidia Taifa kwa hundred percent. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoka hapo niongelee miundombinu ya maji chakavu Dar es Salaam. Kwa kweli miundombinu ya maji Dar es Salaam inahitaji ukarabati mkubwa. Miundombinu mingi imechakaa, Waziri ni shahidi kwa sababu anaishi Dar es Salaam na asilimia 90 ya Wabunge wote hapa mnaishi Dar es Salaam, mnayaona mabomba yanavyopasuka na kuleta disturbance kubwa hasa kwenye barabara. Unakuta barabara zote zimejaa maji utafikiri kuna mvua yaani saa zote Dar es Salaam ni mafuriko kwa sababu ya miundombinu ya maji kuchakaa. Naomba kabisa Waziri anapokuja kuhitimisha atuambie kwa bajeti hiyo aliyoitenga huo uchakavu ataurekebisha vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niongelee bajeti ya maji. Wizara hii naona kama vile haipewi kipaumbele kwa sababu tumeona bajeti ya maendeleo imetekelezwa kwa asilimia 19 tu. Kwanza atueleze kwa nini bajeti imepungua kutoka shilingi bilioni 900 mpaka shilingi bilioni 600? Vilevile atueleze kwamba hii Wizara kumbe siyo kipaumbele? Kama siyo kipaumbele basi na Waziri ni mshauri wa Rais amuulize kwamba hii Wizara mimi unanifanyaje? Kwa nini kati ya shilingi bilioni 900 za maendeleo apewe shilingi bilioni 150 ambayo sawa na asilimia 19 na wakati anaona kabisa tatizo la maji linavyokuwa kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia Wizara ya Miundombinu hapa imepewa asilimia 84, kumbe kuna Wizara ambazo zinapewa bajeti kubwa na kipaumbele. Hii miundombinu inapewa kipaumbele sio vibaya, lakini maji nayo yapewe kipaumbele. Kwa sababu Wizara ya Miundombinu na Uchukuzi ndio mnanunua ndege, kujenga barabara, sawa ndege ni nzuri kupanda lakini utapandaje ndege kama hujaoga? Hivi kweli utapanda ndege kama hujaoga hiyo ndege itakuwaje? Utapita kwenye barabara hujaoga? Mimi nashangaa hiyo Bombardierkama tunapanda hatujaoga inabidi sasa tuwe na perfume ndani kwa sababu maji hayatoki na maeneo mengine ndio maji hakuna kabisa. Sawa ndege sisi imetu-savesana lakini inakuwaje tupande kule bila kuoga. Mimi naona hiyo bajeti iangaliwe upya.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee pia miradi mingi ya maji kutegemea fedha za wahisani. Kwanza, sasa hivi naona kabisa mahusiano ya sisi na wahisani siyo mazuri na wala hawatuletei hela. Sasa mnavyotuambia hizi pesa nyingi tutegemee miradi ya wahisani, kwa mfano, huo mradi unaoendelea Dar es Salaam umetengewa dola za Kimarekani bilioni 32 wanasema hizo fedha zinatoka World Bank, je, zitakuja?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimeona kwenye Kitabu cha IV cha maendeleo naona kabisa Mkoa wa Dar es Salaam mmeandika water and sanitation shilingi milioni 900 lakini zote ni fedha za nje, hivi unategemeaje hela kutoka kwa mwenzio? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa mkubwa kama ule maana wote mnakaa kule Dar es Salaam lakini hela za ndani hamna mnategemea hela za nje tu, shilingi milioni 900 zote zitoke nje, kama wasipoleta? Sasa hivi wana vikwazo kibao hawaleti sasa hivi.Sasa nyie mnavyotegemea hela hizo shilingi milioni 900 zitoke nje inakuwaje? Sasa wasipoleta Waziri atatueleza kwa sababu miradi yetu itakuwa inakwama, yeye anategemea tu wafadhili, awaulize kwa nini hawamtengei fedha za ndani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niende pia kwenye miradi hii iliyoainishwa kwenye ukurasa wa 72 na 73, uchimbaji wa visima Mpera na Kimbiji. Hivi visima toka vianze kuchimbwa sasa hivi ni miaka saba, hiyo miradi kwa nini inasuasua namna hiyo? Mimi mwenyewe nikiwa kama Mthamini, tulishathamini kule mwaka 2007 ili watu waondoke ili vile visima vichimbwe, leo ni miaka mingapi?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri anaendelea kutuambia hapa Kimbiji na Mpera sijui vita-save Gongo la Mboto, Chanika, Keko, hii siyo kweli, huu mradi unakamilika lini mpaka leo haujakamilika? Miaka saba sasa huu mradi anatuambia tu unakamilika, upembuzi yakinifu umekuwa sawa na anatafuta hela. Naomba atafute hela sehemu nyingine tuelewe, huko anakotafuta sasa hivi siko.Atafute sehemu nyingine atuambie anazitafuta wapi na atuambie huu mradi unakamilika lini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna mradi huu wa ukarabati na upanuzi wa mfumo wa kusambaza maji safi, hapa amesema kabisa kwamba sehemu ambayo hakuna miundombinu hiyo atasambaza na amesema umetengewa dola za Kimarekani milioni 32. Vijiji alivyovitaja ni Changanyikeni, Makongo Juu, Kiluvya, Makabe, Msakuzi na vingine vingi lakini anategemea hela ya Benki ya Dunia, yaleyale yanakuja, asipozipata? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa hivi sisi tunashangaa utekelezaji wa huu mradi unakuwaje? Huu mradi unatakiwa utekelezwe mwaka huu na sisi tunakaa huko huko na hatujaona hata hilo bomba lenyewe, lakini hapa anatuambia anaanza kujenga matanki na kadhalika. Sisi tunasema kabisa bwana kama huo mradi umefeli atueleze tuelewe kwa sababu mambo ya kuanza kutudanganya hapa hapana. Akija hapa kuhitimisha atuambie kabisa kwamba huu mradi bwana mpaka sasa hivi tunaendelea kutafuta hela tujue na sisi tutaendaje kutafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niendelee kusema kwamba, inaonekana kabisa bajeti ya maji hapa ni tatizo na kama ni tatizo basi wananchi wafundishwe njia nyingine sasa za kuvuna maji ya mvua. Vibali vya ujenzi vyote vielekeze nyumba kuwa na mfumo wa kuvuna maji ya mvua la sivyo mtu asijenge…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Salma Mwasa muda wako umekwisha.