Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mweyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina jambo dogo tu la kumkumbusha Mheshimiwa Maghembe, kwanza kabla ya yote najua moja ya mambo ambayo yanachangia kutoendelea kwenye sekta ya utalii ni pamoja na miundombinu. Mimi naomba nikuambie ni mtalii mzuri tu hata Easter yangu nilienda kula pale Ruaha National Park.

Mheshimiwa Waziri na Wizara ya Miundombinu hakikisheni hizi mbuga zetu zinapitika vizuri, barabara mpaka katika maeneo ya mbuga yapitike vizuri ili sasa tuweze kuvutia watalii wengi zaidi. Hilo ni jambo la msingi sana kama tunataka kupunguza kwanza gharama na kuhakikisha kunakuwa na watalii wa ndani zaidi; na wa nje kufika kirahisi katika mbuga zetu za wanyama, hilo ni jambo lingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niende jimboni; Mheshimiwa Waziri nilichangia mwaka jana na mwaka huu narudia, mimi napenda sana uhifadhi, lakini haya mambo yanategemeana na nilisema hatuwezi tukalinda mbuga zetu kwa mtutu. Watu ambao wanaweza wakawa walinzi wazuri ni wananchi wanaozunguka hizi hifadhi. Kule kwetu Mara, jimboni kwangu tuna Mbuga ya Serengeti lakini kila siku tembo wamekuwa wakitoka wakila mazao ya wananchi, wakiharibu nyumba za wananchi na kuua wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri hili nimekuwa nikilizungumzia sana. ukienda Kunzugu, Miale, Nyamatoke na maeneo mengine, ukija kule kwa kaka yangu Boni pia jimboni kwake na kwenyewe kuna matatizo hayo hayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.