Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na utalii. Tanzania kama nchi ina vivutio vingi sana vya utalii kwenye maeneo mengi mbalimbali lakini tatizo lililopo ni vivutio vingi kutojulikana, hivyo nashauri:-

(a) Kuwa na chombo mahsusi kwa ajili ya kutangaza vivutio hivi, chombo hiki kiwe na jukumu la kubaini vivutio hivi maeneo viliko na kuvitangaza kwenye maeneo mbalimbali duniani kupitia Balozi zetu na namna nyingine zinazowezekana. TTB ibaki na usimamizi na uratibu na kuacha chombo hicho maalum kibaki na kazi ya kutangaza utalii.

(b) Wizara iwekeze pesa za kutosha katika utangazaji wa utalii badala ya kufikiria kupata mapato ya kutosha kupitia utalii bila kuwekeza katika utangazaji. Mfano, vivutio vilivyoko Wilayani Ukerewe kama vile:-

(i) Jiwe linalocheza la Nyabureke;
(ii) Makazi ya Chifu Lukumbuzya;
(iii) Mapango ya Handebezyo;
(iv) Kaburi la mtunzi wa kwanza wa vitabu Hamis Kitelezya; na
(v) Pwani ya Rubya yenye mchanga mweupe na adimu sana na kadhalika.

(c) Mapato yanayotokana na maliasili yawafaidishe wananchi wanaoishi jirani na hifadhi hizi. Jambo hili litafanya watu hawa wajione ni sehemu ya hifadhi hizi na hivyo kushiriki kuzitunza bila kinyongo.

(d) Miundombinu kama barabara zinazoekea kwenye vivutio hivi vya utalii iboreshwe ili watu wenye nia ya kuvitembelea waweze kuvifikia bila matatizo jambo litakalowahamasisha kuendelea kutembelea vivuto hivi.