Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ni kuhusu fidia ya watu wanaouawa na kujeruhiwa na wanyama wakali kama mamba katika kijiji cha Makaule na Kazamoyo Tunduru. Watu waliouawa na fisi katika kijiji cha Jiungeni na Mchesi Wilaya ya Tunduru bado hawajalipwa fidia hadi leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia kwa watu walioharibiwa mazao yao na wanyama wakali hasa tembo katika kijiji vya Mchoteka, Wenje, Likweso, Walasi, Nasomba, Kazamoyo, Lukumbule, Makande, Mtina, Angalia, Malumba, Misyaji na maeneo mengine ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru hadi leo hawajalipwa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro wa mipaka na hifadhi katika kijiji cha Misyale na Ukala, ambapo askari walizoa vyakula vya wananchi wanaolima katika maeneo ya hifadhi na kuuza bila kuwachukulia hatua za kisheria. Maeneo mengine yenye migogoro ni Hifadhi ya Misitu Misedula na kijiji cha Msinji katika kata ya Ligoma. Ni vyema baadhi ya maeneo yakagawiwa kwa ajili ya kilimo na huduma za jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kuna vivutio vingi sana ambavyo vinaweza vikatangazwa na kutembelewa na watalii na kuliingizia Taifa pato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TFS wanamaliza misitu kwa kutoa vibali ovyo vya mbao na uvunaji wa magogo bila kujali athari za mazingira. TFS wana mahusiano mabaya na wananchi waliopo karibu na hifadhi za misitu. TFS wameshiriki kuhujumu misitu karibu maeneo yote yenye hifadhi za misitu. Misitu ya asili inaisha kama TFS hawataacha kulinda vizuri misitu yetu.