Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na watendaji wa Wizara hii. Naomba kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina nia ya kupanua eneo la Hifadhi ya Taifa ya Selous hadi Wilaya ya Mbinga katika Kata za Litumbandyosi na Ruanda. Fukuto la migogoro ya mipaka katika eneo hili limekwishaanza kujitokeza. Hivyo naishauri Wizara ichukue hatua za haraka kwenda kuweka vizuri mipaka katika kata hizo za Litumbandyosi na Ruanda ili kuepusha migogoro hiyo inayofukuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa katika upanuzi wa hifadhi kwa niaba ya wananchi wa kata hizo naomba mipaka ikarekebishwe ili yale maeneo yanayolimwa waweze kuachiwa waendelee na shughuli zao za kiuchumi

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke wazi fursa zilizopo katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Misitu (Tanzania Forest Fund) ili wananchi wapate kunufaika nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Mbinga katika kijiji cha Mbuji, Kata ya Mbuji yapo mawe makubwa mawili ambayo inasadikika kuwa mawe hayo ni Bibi na Bwana, kwa maana kwamba kuna jiwe la kiume na jiwe la kike. Katika mawe hayo unafanyika utalii ambao si rasmi na miaka ya hivi karibuni kuna mzungu alidondoka kwenye jiwe mojawapo hadi kupoteza maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mawe hayo kuna viumbe hai wanaoishi ambao wanafanana na binadamu isipokuwa wao ni wafupi sana. Viumbe hao wanafahamika kama “VIBUTA” kwa lugha ya Kimatengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara ikafanye utafiti katika mawe hayo ili kubaini viumbe hivyo na kubaini fursa nyingine za kitalii. Inasadikika kuwa viumbe hao wanapatikana pia katika nchi ya Australia. Naomba kuwasilisha.