Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kunipa uhai na kuweza kuchangia hoja iliyoko mezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro kati ya hifadhi na wananchi imekuwa sugu na ya muda mrefu. Nilipokuwa Mjumbe wa Bodi ya TANAPA ulitayarishwa mpango mkakati wa kutatua migogoro hiyo, watendaji wa TANAPA waliainisha maeneo yote yenye migogoro na wananchi, yaliwasilishwa kwenye Bodi ya Wadhamini na maamuzi yalifikiwa kama ifuatavyo:-

(a) Maeneo yenye migogoro na ambayo hayana madhara yoyote kwa hifadhi au ekolojia ya eneo la hifadhi waachiwe wananchi na mipaka irekebishwe.

(b) Maeneo yale yenye migogoro na uwepo wa human activities kuhatarisha bionuai na ekolojia ya hifadhi, wananchi washawishiwe kuachia maeneo hayo na Serikali iwape ardhi nyingine na kuwalipa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maamuzi haya hayakutekelezwa kwa sababu muda mfupi baadae aliyekuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Pinda aliunda Tume ya kuchunguza migogoro yote ya ardhi na kutoa mapendekezo, baadae tena Waziri wa Ardhi naye aliunda Tume kwa jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha kwa Serikali kushindwa kutoa uamuzi kwa jambo nyeti linalogusa hisia za jamii. Serikali ichukue maamuzi magumu ya kutatua kero hii badala ya kujificha nyuma ya Tume na Kamati zinazoundwa kila mara ili tu isifanye maamuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro hii sasa na zaidi ya miaka kumi tangu nimeanza kuisikia, ni matumaini yangu kwamba kabla Awamu ya Tano haijamaliza muda wake wa miaka mitano itaacha alama ya kudumu ya kutatua kero hii.