Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, sekta hii muhimu kwa uchumi wa Taifa. Kiwango cha kutangaza utalii kipo chini hali ya kuwa na tozo nyingi zinazotozwa zikidaiwa matumizi yake ni promotion kupitia Bodi ya Utalii mfano watalii wanalipa dola moja per head wanapolala kwenye hoteli per night na zinapelekwa Bodi ya Utalii. Matozo mengi yanafanya watalii wengi kukimbilia Kenya na mpaka Kenya wana-captalize Mlima Kilimanjaro ni wao na watalii wanafikia kwao due to number of charges zisizo na sababu. Katika eneo la matangazo mfano ndege za Kenya zimeandikwa Kilimanjaro na zinakwenda nchi nyingi duniani, kwa hiyo, ni rahisi kuwaaminisha wageni kuwa Mlima Kilimanjaro upo Kenya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwe na strategies nzuri za ku-promote utalii na kuondoa siasa kama za kusema tunanunua ndege kubwa ya Dreamliner itakayoruka Ulaya mpaka Kilimanjaro ikiwa na watalii is this a strategy? Hapo hapo mkoa wenye utalii umejaa siasa za chuki mpaka kukera wageni, kwa mfano RC kaweka mtu ndani muda mrefu kwa zaidi ya miezi minne bila dhamana kwa kesi ambayo ina dhamana, yote haya wageni wanayaona na wanatushushia value.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA wafanye kazi na kupunguza matumizi yasiyo na lazima. Kwa mfano kuna Mawaziri walikuwa wanatumia mali za TANAPA kama magari, ndege kama mali zao binafsi na zikatumika mpaka kwenye kampeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Faru John na Faru Fausta ambapo Faru Fausta gharama za matunzo yake ni kubwa wakati matukio ya ujangili ni makubwa na yanaendelea. Hata taarifa ya Faru John namna alivyopotea inajulikana ila imefunikwa funikwa na imepita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoteli nyingi za kigeni zina- charge gharama kubwa na masharti yake ni magumu. Hoteli hizi zinawalenga hata wazawa ambapo huendi bila appointment na ndiyo hao faru wanapotelea kwenye hizo hizo hoteli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa maliasili na nishati, matumizi ya mkaa yanaendelea kuongezeka nchini na hii inatokana na kupanda kwa gharama za gesi. Serikali huwezi kuhimiza matumizi ya nishati mbadala wakati gesi na umeme gharama yake ipo juu. Makaa ya mawe,
wawekezaji kama Dangote amepewa achimbe kwa nini yasitumike pia kwa wazawa kama nishati ili waache kuchoma mkaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro maeneo ya hifadhi namna ambayo wawekezaji wanapewa vipaumbele kuliko wazawa na mwisho huwa ni migogoro isiyoisha. Wawekezaji wana viwanja vidogo vya ndege ndani ya hifadhi mfano Serengeti wanavifanyia nini kama siyo vinatumika kuhujumu uchumi wetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi ambayo ipo Mtwara tulihakikishiwa kuwa itakuwa muarobaini wa mambo mengi ikiwemo matumizi ya nyumbani ili kunusuru ukataji misitu, ikiwa ni pamoja na matumizi ya gesi ya majumbani na bei itakuwa chini. Kuna sehemu kama Dar es Salaam yalitandazwa mabomba ya gesi mitaani lakini hakuna lolote, mkaa tani na maelfu ya tani kila siku yanapelekwa Dar es Salaam.