Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna madini ya chokaa yaliyoko mbuga ya wanyama Moyowosi eneo la Kakonko. TCCIA na wadau wa maendeleo walileta ombi Wizarani kupitia DCC ili kuongeza eneo la kilometa 15 kuingia mbugani kusababisha eneo lenye chokaa kuwa nje ya mbuga na kuwafanya wananchi wanufaike na chokaa hiyo lakini hadi sasa hakuna majibu yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wizara ijikite katika kutangaza utalii nje na ndani ya nchi. Kiasi cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya kutangaza utalii hasa nje ya nchi hakitoshi. Nchi ya Kenya wamefanya vizuri kwenye matangazo ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wimbi la mauaji ya wananchi ndani ya hifadhi kana kwamba wanyama ni bora kuliko wananchi. Hali hii inatupunguzia heshima kimataifa na kitaifa. Uwekwe utaratibu mzuri wa kuhakikisha hakuna raia/mwananchi anayepoteza maisha kwa kukutwa kwenye hifadhi ya wanyama au misitu. Kuua watu marufuku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na mauaji ya wananchi/raia kuna mifugo inayoingia kwenye hifadhi na kuuawa/kuzuiliwa na hivyo ama kutozwa faini au kuuzwa kwa njia ya mnada ambapo fedha zinakuwa za Serikali. Huu ni wizi wa Serikali. Hata kama wamekosea kuingiza mifugo kwenye hifadhi bado mifugo ni mali yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tozo nyingi kwenye sekta ya utalii; VAT iliyoongezwa mwaka jana kwenye utalii kwa mtalii kulipia kulichangia kupunguza idadi ya watalii waliokuja nchini kwani nchi jirani yetu hawana hiyo VAT na hivyo watalii wengi kukimbilia nchi hizo kwa sababu ya gharama nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi zinachukua eneo kubwa sana na mengine hazifanani na idadi ya wanyama waliopo. Hali hii ikilinganishwa na ongezeko la watu husababisha wananchi kukosa ardhi ya kilimo na mifugo. Nashauri ifanyike tathmini kwenye hifadhi zote kuona hali ya hifadhi na mahitaji ya ardhi kwa wananchi wanaozunguka hifadhi ili hifadhi zisogezwe ndani zaidi kuwezesha wananchi kupata ardhi. Hii itapunguza ugomvi kati ya wafugaji na hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ijipange vizuri katika zoezi la kuzuia matumizi ya mkaa bila kuja na nishati mbadala. Bei ya gesi na umeme viko juu kiasi kwamba mwananchi hawezi kutumia gesi/umeme kwa kupikia, hataweza kumudu gharama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TFS Kakonko, Jimbo la Buyungu. TFS wanatesa wananchi Wilayani Kakonko kwa kukamata wananchi wenye hata mbao moja au gunia la mkaa. Hali hii haikubaliki kwani bado wananchi wanahitaji kujenga, kutengeza samani na kadhalika. Mateso haya hayavumiliki.