Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri ya kuongoza Wizara hii muhimu. Aidha, nampongeza Katibu Mkuu na watumishi wa Wizara kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Idara ya Malikale ishirikiane na Halmshauri ya Karagwe na Ofisi ya Mbunge kuendeleza maeneo ya Malikale ikiwemo yaliyokuwa Makao ya Chifu Rumanyika. Mara nyingi nimekuja kuwaona Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri juu ya jambo hili, naomba msaada kwa niaba ya wananchi wa Karagwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iweke utaratibu wa ujirani mwema na vijiji vinavyopakana na Pori la Akiba la Kimisi kwenye Kata za Rugu, Nyakasimbi, Nyakakika, Nyakabanga na Bweranyange kwa kusaidia kuboresha sekta ya elimu hasa kusaidia ujenzi wa madarasa ya shule za msingi, nyumba za walimu, matundu ya vyoo na kuchimba visima vya maji. Msaada huu ni wa muhimu sana na utasaidia kujenga royalty and sense of community ownership kwa maliasili za umma zilizo kwenye Pori la Akiba la Kimisi badala ya kulitazama with contempt.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri arejee memo yangu niliyomwandikia tarehe 19/05/2017 humu Bungeni juu ya ombi la kuleta wataalam toka Idara ya Utalii kuangalia border belt ya Wilaya za Ngara, Karagwe na Kyerwa ili kufanya ukanda huu ukuze utalii kwa kutumia vivutio vya Malikale, Maporomoko ya Rusumo, Mto Kagera, Ziwa Lwakajunju, Game Hunting kwenye Bonde la Kimisi, Ibanda na Rumanyika Game Reserves na vivutio vingine tulivyojaliwa na Mwenyezi Mungu kwenye border belt hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti,majirani zetu Rwanda on the other side of the border wanajipatia fedha nyingi za kigeni, kwani wametumia fursa asili nilizozitaja kukuza utalii Rwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti,naomba nijibiwe maombi haya kwa maandishi. Ahsante.