Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu na watendaji wao wote wa Wizara kwa kazi nzuri sana wanayofanya. Pili, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuunga mkono hoja hii, naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa misitu kwanza huhifadhi maji, makazi ya viumbe hai, misitu, ni muhimu kwa matumizi mbalimbali ya binadamu kama vile mbao, dawa, chakula, kuni, mkaa na matumizi mengine. Misitu pia hutumika kwa makazi ya binadamu kama Wahadzabe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwa misitu ni muhimu sana, hata hivyo ni vyema wananchi wasifanye uharibifu wa misitu; wasifyeke misitu ovyo na kusababisha jangwa/ukame ambao huleta njaa nchini. Wananchi wasichunge mifugo yao kwenye vyanzo vya maji kwa kuwa maji ni uhai, maendeleo na uchumi wa nchi yetu; wananchi wasijenge kwenye vyanzo vya maji; wananchi wasichome misitu ovyo, kwa kuwa misitu huvuta mvua na bila mvua hakuna chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote haya, Serikali iruhusu wananchi waendelee kutumia/kupikia mkaa na kuni kwa kuwa hawana mbadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawapongeza watendaji wa sekta ya utalii kwa kazi nzuri sana wanayoifanya. Pamoja na pongezi, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sekta ya utalii inachangia Pato la Taifa wajitahidi kuhakikisha kwamba watalii wanaongezeka kila mwaka ili Pato la Taifa liongezeke kuliko hali ilivyo sasa; watalii wapate huduma bora kama vile barabara ziwe nzuri na zinazopitika wakati wote wa masika na kiangazi; kuongeza vivutio kwa watalii ili waweze kuongezeka; huduma ya usafiri iwe bora ili watalii wasisumbuke; waongoza watalii wawe na lugha nzuri na tabia nzuri/njema; na huduma ya chakula na malazi iwe bora kwa watalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watalii siyo lazima wawe wa kutoka nje ya nchi tu, hata utalii wa ndani. Ushauri wangu kwa Serikali, zijengwe hoteli za bei nafuu kwenye mbuga zetu za wanyama ili watalii wa ndani waweze kumudu gharama za malazi na chakula kwenye mbuga zetu za wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti,naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.