Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii napende kuchangia mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya uhifadhi na utalii ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu. Sekta ya utalii inachangia takribani asilimia 17.5 ya uchumi wa Tanzania. Kuna umuhimu sasa Serikali itie mkazo katika kuhakikisha sekta hii ya utalii inafanya vizuri ili kuongeza mapato na kukuza uchumi wetu wa Tanzania. Serikali inatakiwa ifanye jitihada kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 idadi ya watalii nchini iwe imeongezeka kufikia milioni mbili ambapo itaongezeka mpaka asilimia 20 - 25 katika uchumi wa Tanzania. Kuna umuhimu pia kuweka jitihada/mkazo kwenye utalii wa fukwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara/Serikali iweke mikakati mizuri katika kuhamasisha utalii wa ndani kwa kuongeza matangazo katika sehemu muhimu ili wananchi watembelee maeneo ya utalii kama Ruaha National Park kule Iringa, wajulishwe uzuri wa kule, mfano kuna simba wanaotembea kwa makundi makubwa ambayo ni kivutio kikubwa. Mbuga ya Kitulo kule Mkoa wa Njombe, mbuga yenye maua mengi ya kila aina tuitangaze ili kuweza kupata watalii wengi, ni kivutio cha aina yake.

Mhesimiwa Mwenyekiti, Serikali pia iongeze mbinu za kupambana na ujangili ili tuweze kulinda wanyama wetu kama faru, tembo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nashauri kwamba elimu ya uhifadhi itolewe kwa wananchi, waelewe faida ya uwepo wa mapori ya hifadhi. Kwa kufanya hivi tutaweza kuepusha migogoro ya wananchi na hifadhi kama kule Loliondo na maeneo mengine. Wahifadhi wa pori watoke kwa wananchi kutoa elimu ya uhifadhi, wasikae maofisini tu na Serikali iboreshe mikakati ya kuvutia watalii wengi zaidi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Utalii, TANAPA pamoja na NCAA waendelee kutangaza vivutio vya utalii kwa kasi kubwa zaidi. Serikali/Wizara iweke mabango mengi na kuyasambaza kwenye maeneo muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, Serikali iwapatie budget/pesa za kutosha Wizara hii ili waweze kufanikisha shughuli zilizokusudiwa kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, naunga mkono hoja.