Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

HE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nishati ya mkaa holela ni hatari kwa ustawi wa nchi yetu. Tukisubiri gesi au umeme itatuchukua karne nyingi hadi kufikia wananchi wote kuachana na mkaa wa kuni.

Hivyo basi, kwa kuwa tangu mwaka 2012 kuna shirika linalojishughulisha na mafunzo kwa wanavijiji vipatavyo 30 vya Wilaya za Kilosa, Morogoro na Mvomero uchomaji wa mkaa endelevu kwa kutenga misitu ya kuchoma mkaa. Shirika hilo linafadhiliwa na watu kutoka nje ya nchi na tija ni kubwa na ndiyo mkombozi wa misitu yetu. Hivyo Serikali itenge bajeti ya kuwezesha Halmashauri kufundisha miradi ya mkaa endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine napenda kupata majibu ya Serikali kuhusu madhara wanayopata wananchi wa Jimbo la Mlimba, kata ya Utengule na Msagati kwa kuchomewa nyumba, vyakula na kadhalika. Jambo hilo linafanywa na wamiliki na kitalu cha uwindaji (Kilombero North Safari). Tumefuatilia sana kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilombero ambapo ufumbuzi haujapatikana wa kuainisha mipaka ili wananchi waishi kwa amani katika vijiji vyao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kuna timu ya pamoja iko Wilaya ya Malinyi na Ulanga inarekebisha mipaka ya eneo oevu (Ramsar Site) ambao umeleta usumbufu kwa kuwa hawashirikishi wananchi na kuweka mipaka upya na hata wanapowashirikisha hawafikii muafaka, kwani wanalazimisha mipaka.

Hivyo basi, kazi hiyo inayoendelea huko haina tija bali ni kukuza migogoro. Ushauri wangu, naomba Mheshimiwa Waziri afanye ziara Mlimba na maeneo yote ya Bonde oevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kupata majibu ya Serikali, ni kwa nini ndani ya Bonde la Oevu mmeacha ng’ombe wengi tena inasemekana ni ng’ombe wa viongozi? Badala yake mnawanyanyasa wafugaji katika vijiji na kuwaacha wenye makundi makubwa ya ng’ombe wakiharibu Bonde la Kilombero huku mkipokea misaada ya fedha toka nje kwa madai mnahifadhi ardhi oevu?