Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Namtumbo tunashukuru sana kwa kupewa heshima kwa mwakilishi wao kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Imani hiyo ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hakika itazaa imani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa MIVARAF unaihusu sana Wilaya ya Namtumbo ambayo wakazi wake ni wakulima kwa zaidi ya asilimia tisini. Ujenzi wa miundombinu ya barabara za kuwezesha mazao ya wakulima kuyafikia masoko pamoja na ujenzi wa maghala ya kuhifadhi mazao ni muhimu. Shughuli zinazofanyika katika mradi wa MIVARAF ni muhimu sana kwa wakulima wa Namtumbo. Nitashukuru kujulishwa mradi huo unaanza kutekelezwa lini Wilayani Namtumbo na una bajeti ya kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti,naunga mkono hoja ya bajeti iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa Bungeni kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti,naomba kuwasilisha.