Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kuwapongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Maghembe na Naibu wake Engineer Ramo pamoja na timu nzima ya Wizara kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya katika Wizara ya Maliasili.

Mheshimiwa Mwenyekiti mchango wangu uko katika maeneo mawili, kwanza ni kuhusu utalii wa utamaduni, lakini pili nimalizie kuhusu suala la Vazi la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kukiri kabisa kwamba tuna vivutio vingi vya utalii wa utamaduni katika nchi yetu kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge wenzangu, lakini Wizara yetu ina kazi kubwa, iko katika mchakato wa kutekeleza Mkataba wa UNESCO wa mwaka 2003 ambao unahusu Urithi wa Utamaduni Usioshikika na ule mkataba wa mwaka 2005 wa Kulindwa na Kukuzwa kwa Uanuai wa Kujieleza Kiutamaduni.

Sasa tunachofanya sisi Wizara ni kukusanya taarifa na tafiti kutoka kwa wadau mbalimbali zikiwemo Halmashauri, na taarifa hizi zinahusu maeneo ya kihistoria, kimila, kidesturi na vivutio vya utalii wa kiutamaduni.

Mheshimiwa Mwenyekiti katika zoezi hili tunashirikiana kwa karibu kabisa na Wizara ya Maliasili, Kitengo cha Malikale pamoja na TAMISEMI na zoezi hili ni endelevu na uendelevu wake utaona kwamba kuanzia mwezi Agosti, 2016 hadi sasa tumeshapata vivutio vipya kutoka Halmashauri 35 na Mikoa 19. Lengo kumbwa ni kuzitumia taarifa hizi katika kuwasaidia wananchi kuweza kutumia utalii wa kiutamaduni kuongeza kipato. Kwa hiyo, nitoe wito kwamba Halmashauri zote ziendelee na zoezi hili na tuna dhamira kubwa ya kutumia baadhi ya mila na desturi zetu katika kuzipeleka kwenye orodha wa Urithi wa Utamaduni wa Dunia. Kwa mfano, mila na desturi ya jando na unyago ambayo iko katika Mikoa ya Kusini na Mikoa ya Ukanda wa Pwani kama vile Wamakonde; na ile mila ya Wamasai ya kurithisha ngazi ya rika ya kipengele cha Engpaata Yunoto na Olng’esher. Kwa hiyo, vivutio hivi vikiingia katika Orodha ya Urithi wa Dunia vitasaidia sana kuwa vivutio vya utalii wa utamaduni katika yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mimi binafsi nikiri kwamba nimeshawahi kutembelea baadhi ya vivutio na niseme tu kwamba bado Halmashauri zetu zina kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba zinaboresha mazingira katika maeneo yale ya vivutio. Kwa mfano, Halmshauri hizi zihakikishe kwamba kunakuwepo na vyoo, barabara nzuri, maeneo ya kulia chakula kwa sababu vivutio vingine vingi viko katika maeno ya maporini, lakini ni vizuri sana. Kwa mfano nilishawahi kufika katika kichuguu ambacho kinacheza kule Babati, kunahitajika maboresho ili kusudi watalii wengi waweze kufika. Nishauri tu Halmashauri zione umuhimu wa kutenga bajeti ili kusudi kuweza kuboresha maeneo hayo Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa upande mwingine nizishauri halmashauri pia ziwatumie wacheza filamu pamoja na waigizaji katika maeneo yao kwa kuwapa mikopo ili kusudi waweze kucheza filamu za…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.