Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

HE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia hoja hii ya Wizara ya Elimu. Nami niungane na Watanzania wenzangu kuwapatia pole wazazi wa Arusha kwa kufiwa na watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na miradi ya Wizara ya Elimu hususani fedha za miradi kutopelekwa kwa wakati. Nikiwa mwanakamati wakati tulipotembelea miradi tuligundua kwamba fedha haziendi kwenye miradi au kama zinakwenda basi zinakwenda kwa kuchelewa. Kwa mfano, mradi wa Chuo Kikuu cha Sokoine, mwaka jana walitengewa shilingi bilioni nne lakini mpaka Machi fedha hizi hazikwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo walitengewa shilingi bilioni
9.4 hadi Machi fedha hizi zilikuwa hazijaenda. Niwaombe Waziri wa Elimu na Naibu wake fedha hizi zitakapotengwa safari hii mhakikishe zinakwenda kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee campus ya Mloganzila. Campus hii kwa kweli ni mfano, imekamilika mwaka jana na hii ina vifaa vyote vya kisasa lakini hakuna watumishi. Niombe Serikali kuhakikisha watumishi wanapatikana kwa ajili ya campus hii kwa sababu ni aibu kwetu sisi Watanzania kuwa na campus kama hii halafu haina wafanyakazi, hii inaonesha kwamba hatukuwa tumejipanga. Kwa hiyo, niiombe Serikali ipeleke watumishi katika campus hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niongelee suala la watoto wa kike kurudi shuleni au kutorudi shuleni baada ya kupata ujauzito. Mimi kama mama na kwa yeyote ambaye ana uchungu wa mtoto au uchungu wa kuzaa, nafikiri jukumu la huyu mtu au la mzazi huyu ni kutetea kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito kwa sababu anapata ujauzito huu kwa kurubuniwa si kwa kutaka na kwa mazingira magumu na wengi wanakuwa hawana fedha, hiyo ndiyo inayowasababishia kupata ujauzito. Kwa maana hiyo, naiomba Serikali watoto hawa warudi shuleni mara baada ya kujifungua.

TAARIFA...

HE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza naikataa taarifa hii kwa sababu akina baba ndiyo mnaosababisha matatizo haya ya watoto wetu kupata ujauzito.

TAARIFA...

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naipokea taarifa hiyo. Kwa asilimia kubwa hata kama sheria imekwishawekwa watu hawachukuliwi hatua yoyote, wanaopata matatizo ni watoto wetu wa kike, ndiyo wanaoathirika. Kwa hiyo, niiombe Serikali kulifikiria suala hilo kwa sababu imekuwa ina kigugumizi kulipitisha jambo hili. Niiombe tafadhali Mheshimiwa Waziri atusikilize safari hii walipokee suala hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la shule za private. Mimi pia na- declare interest kwamba, nina shule ya private, tena shule hii ni ya watoto yatima. Kwa kweli watu wa shule za private wanapata matatizo mengi sana. Tatizo la kwanza ni kodi nyingi halafu wanafuatiliwa sana wakati watu wa private wanakuwa wana vigezo vyote tofauti na shule za Serikali. Wana Walimu wazuri ambao wamegharamiwa kwa hela nyingi na wanalipwa vizuri, wana vifaa vyote vya shule, wananunua vitabu vyote vya kutosha kwa ajili ya wanafunzi lakini bado Serikali inawabana.