Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza kwa dhati Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. J. P. Magufuli kwa kuonesha nia na uwezo mkubwa wa kuiongoza nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kumpongeza Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri wake wote. Naomba waongeze juhudi na misimamo yao katika kuongoza Wizara zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa wananchi kujiunga na matumizi ya soko la Marekani bila ya ushuru chini ya mpango wa AGOA. Hata hivyo, Serikali haikueleza namna itakavyochukua hatua za kuwaelimisha wananchi kujiunga na mpango huo. Ni vyema Serikali ikawaelekeza na kuwatayarisha wananchi ili kuwapa ujuzi na uelewa wa soko hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo hayo, naunga mkono hoja. Ahsante.