Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jitihada zenu za kuboresha sekta ya elimu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi, nilishauri na Baraza la Madiwani likapitisha hoja yangu ya kuwa na malengo ya na A-level kila tarafa. Karagwe tuna tarafa tano lakini ipo A- level moja tu. Ninaomba Wizara itusaidie kwenye vipaumbele vya kukamilisha malengo ya A-level mbili kama ifuatavyo:-

Nyaboyonza sekondari bwalo moja, jiko moja, bweni moja na vitanda; Kituntu sekondari bweni la wavulana; Bisheshe sekondari si A-level ila sekondari hii tunaomba msaada ikamilike haraka kusaidia watoto wanaotembea umbali mrefu kupata elimu ya sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupanda madaraja imekuwa tatizo kwa Karagwe, mapunjo ya mishahara, walimu wengi Karagwe kuanzia mwaka 2013 hadi sasa hawajalipwa hiyo fedha na madeni tayari yamehakikiwa na orodha ya walimu wanaodai CWT walipewa orodha hiyo mpaka sasa walimu hawajui muafaka ni lini wanalipwa.

Aidha, kwa walimu Karagwe kuna usugu wa kutopandishwa madaraja kwa zaidi ya 13. Utakapokuja kuhitimisha naomba uniambie tatizo hili linasababishwa na nini? Kwa nini mshahara unachelewa kurekebishwa ili uendane na tarehe ya kupandishwa daraja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni yanayodaiwa na walimu yanakuwa na makato, na hii si haki kwa walimu. Serikali iweke utaratibu wa kulipa riba kwa madeni ya walimu ili walimu hawa wapate time value of money pamoja na consideration ya inflation (mfumuko wa bei).

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejitahidi sana kupitia Mfuko wa Jimbo na michango yangu binafsi kusukuma kazi za uboreshaji wa elimu ya msingi Karagwe. Naomba Wizara iingilie kati kwenye shule ya msingi Ahakanya na shule ya msingi Rwentuhe ambapo walimu na wanafunzi wanasomea kwenye miti. Tayari nilishampa picha za shule hizi Mheshimiwa Waziri Profesa Joyce Ndalichako. Pia shule ya msingi Rweizinga kwenye kijiji cha Mgurika, kata ya Bweranyange kuna baadhi ya wanafunzi wanasomea kwenye darasa la udongo lililoezekwa na majani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi bilioni mbili za kupanua Chuo cha VETA cha KDVTC hazijafika kwenye chuo, ninaomba Wizara itusaidie kupata fedha hizi.