Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia Wizara hii katika maeneo matatu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, uundwaji wa vikundi vya kijamii (SACCOS). Mpaka sasa ni vikundi vichache vimeweza kusajiliwa kutokana na uelewa mdogo na kutotembelewa na wahusika kwa maana ya viongozi wa ushirika kutoka katika Halmashauri zetu. Mpango huu wa kusaidia vijiji shilingi milioni 50 binafsi najua kuna vikundi havitakuwa na sifa kutokana na ugumu huo wa usajili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni habari. Kama nchi tume-sign mikataba mbalimbali ya haki ya kupata na kutoa habari kwa wananchi. Masikitiko yangu ni kwamba, Serikali imezuia vyombo binafsi kuonyesha, kuandika shughuli za Bunge zinazoendelea kwa kigezo cha kuwa na Bunge TV ambayo kimsingi haionyeshi na kama inaonyesha, inaonyesha kwa upendeleo. Isitoshe kuna magazeti yamefungiwa na kama Bunge halijajua makosa yao ili vyombo vingine vijifunze. Nashukuru kuleta Muswada wa Sheria ya Vyombo vya Habari, labda utaleta uhuru katika habari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, ni mawasiliano. Tumekuwa na vyombo au Makampuni mengi ya Simu, lakini wasiwasi wangu ni gharama zinazotozwa kwa wananchi. Gharama zinaongezeka katika ununuaji wa vocha na wananchi wengi hawana ujuzi wa kitaalam na kupelekea mwananchi wa kawaida kulipia gharama kubwa sana bila uangalizi wa wataalam watetezi wa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, ni uingizwaji wa simu feki unaofanywa na wafanyabiashara wachache na kujinufaisha na kuacha wananchi wanaathirika kwa ubovu wa simu hizo na hata hasara ya kuharibika baada ya muda mfupi. Nashauri TBS na wadau wanaolinda haki ya mlaji wafanye kazi yao kwa faida ya mwananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, ni masoko. Tumeingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, sijaona kama tumeandaa wananchi wetu hasa wanawake kuingia katika ushindani wa soko. Pia wananchi hawana elimu ya kibiashara hasa ya utalii ukilinganisha na jirani zetu ambao ni washindani wetu.