Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja hii katika haya yafuatayo:-

(i) Katika mgawanyo wa vitabu vya History, Geography na English Book One kwa kidato cha kwanza, Halmashauri ya Mpimbwe haijapata vitabu hivyo.

(ii) Madai na madaraja ya walimu yashughulikiwe kwa haraka sana.

(iii) Walimu wasaidiwe vifaa vya kufundishia kama
computers.

(iv) Vitabu vya kidato cha sita, vitabu vya English ni vitano tu.

(v) Suala la uhamisho kwa walimu ni vema likaangaliwa upya na ikiwezekana wapangiwe maeneo yao kwa manufaa ya familia zao.

(vi) Fedha zilizotolewa kama motisha kwa Halmashauri katika Mpango wa P4R, Halmashauri ya Mpimbwe, Jimbo la Kavuu haijapata fedha hizo.

(vii) Mtaala wa elimu uangaliwe upya ili uwezeshe jamii kuendana na mabadiliko ya maendeleo duniani.

(viii) Nakumbusha maombi yangu maalum niliyompatia Mheshimiwa Waziri. Naomba tusaidiwe wananchi wa Jimbo la Kavuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.