Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Serikali kwa kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari (‘O’ level).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu idadi kubwa ya kujiunga na shule za msingi; watoto wameongezeka kwa idadi kubwa sana. Hii imepelekea pia ongezeko la watoto wa sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Serikali na Waheshimiwa Wabunge kwa kununua madawati kwa shule za msingi. Sasa watoto wetu wanasoma vizuri wakiwa wanakaa kwenye madawati. Pongezi kwa kujenga maabara kwa shule za sekondari; pongezi kwa Serikali kwa kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kwa Serikali:-

(a) Serikali iongeze kujenga hostel kwa ajili ya watoto wa shule za sekondari ili kupunguza umbali kwa watoto;

(b) Kuongeza idadi ya walimu hasa walimu wa masomo ya sayansi kwa shule za sekondari;

(c) Kuongeza nyumba za walimu;

(d) Kuongeza kujenga madarasa na ofisi kwa ajili ya walimu wetu;

(e) Posho iwepo kwa walimu wa shule za msingi na sekondari;

(f) Kuongeza mishahara kwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari; na

(g) Kuboresha mazingira ya walimu, kwa mfano, nyumba kuwekewa umeme, maji yawepo shuleni, vifaa vya kufundishia viwepo, usafiri wa shule uwepo kwa kila shule ya msingi na sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja.