Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipongeze sana Wizara kwa kazi kubwa inayofanywa ya kuinua elimu ya Tanzania, bado kuna kama kazi ya kufanya ambayo ninaamini kwa uwezo wenu mtaikabili na kuimaliza mapema. Naomba kuchangia machache yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Buhombe ina changamoto ya uwepo wa Chuo cha VETA, Wilaya hii ipo kwenye rasilimali nyingi zikiwemo misitu (mbao), madini, mifugo (ngozi) ambazo zinaweza kurahisisha kwa kiwango kikubwa ujifunzaji na upatikanaji wa ujenzi (skills) wa kutumia rasilimali hizi ili ziwe zenye faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya yetu ina changamoto ya high school kama nilivyokuja ofisini kwako, naomba sana Mheshimiwa Waziri, shule yetu ya sekondari ya Businda iongezewe mabweni na mabwalo, madarasa na maabara ili shule iwe high school. Kwa sasa hali tuliyonayo wanafunzi wetu wengi wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata elimu ya kidato cha tano na sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukaguzi wa shule, idara ziimarishwe na ninaomba kushauri upatiwe rasilimali za kutosha kwa maana ya miundombinu, rasilimali fedha na watu, nashauri pia wakaguzi walipwe mishahara inayowapasa kama ilivyo kwa Wakuu wa Idara (LSS). Aidha, naomba idara hii, ifanywe kuwa wakala wa kujitegemea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.