Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa wanafunzi kupata elimu bure kuanzia chekechea mpaka kidato cha nne. Pili, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Napongeza Bodi ya Mikopo kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wengi. Kwa upande mwingine kuna wanafunzi ambao wamesoma kwa taabu ya kujilipia au kulipiwa na wazazi wao kwa kusuasua kwa madarasa ya chini, bahati nzuri wanafaulu mpaka Chuo Kikuu lakini kwa bahati mbaya hawapati mikopo kufuatana na vigezo vilivyowekwa. Wanafunzi wengine inabidi waache chuo, kwa sababu ya kukosa malipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwajali na kuwahurumia wanafunzi hawa wanaokosa masomo kwa sababu hawana fedha za kulipia, nashauri inapowezekana wanafunzi wote wapewe mikopo. Mikopo ni mikopo wapewe kwani mikopo hii watailipa hapo baadae. Mheshimiwa Waziri naomba tuwajali pia watoto hawa wahitaji wa elimu ya juu, hawawezi kulipia elimu yao. Serikali yangu sikivu iwaangalie wanafunzi hawa na wenyewe wapewe mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, motisha kwa wanafunzi wanaofaulu alama za juu na hasa wanafunzi wanaochukua masomo ya sayansi, jambo hili likifanyika kuanzia madarasa ya chini, naamini wanafunzi watajituma kusoma, kufaulu na baadaye kulijenga Taifa letu. Jambo hili pia lielekezwe kwa upande wa walimu. Walimu wanaofanya vizuri katika ufundishaji wapatiwe motisha, hii itawapatia moyo kazini mwao na moyo wa utendaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vitabu nashauri iundwe Kamati ndogo ya kupitia vitabu hivi jambo hili litakuwa zuri, kusudi watoto wetu wapate elimu nzuri, kupitia vitabu vilivyoandikwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi wanohitimu vyuo vya VETA ni pongezi kwa Serikali kwa kuwa na mpango wa kuwa na chuo cha VETA kila Wilaya kwa kuwa vyuo hivi vya VETA vinafundisha kwa vitendo, ni vema kila mtoto anapomaliza mafunzo haya aweze kusaidiwa zana ama vifaa vya kuanzia kazi, angalau kidogo ili waweze kujiajiri wenyewe, nashauri jambo hili liangaliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri pia elimu inayotolewa katika vyuo hivi iwe ya kuhitajika katika eneo husika ambapo chuo kipo. Kwa mfano, kwa wastani kila Wilaya hapa Tanzania hata mijini wananchi wengi hutegemea kilimo, kwa kupata kipato cha familia pamoja na kupata chakula chao, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nakuomba na kukushauri kuwa kila Chuo cha VETA kuwe na mkondo wa elimu ya kilimo, kwa sababu ya kuinua familia na viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya nyuma shule hasa za sekondari zilikuwepo zinajulikana kuwa ni shule za kilimo lakini sasa hivi hakuna, nashauri utaratibu huu uanze tena ili kusudi wanafunzi baada ya kupata elimu ya sekondari na kama hakubahatika kwenda elimu ya juu, aweze kujitegemea kwa elimu ya kutosha ya vitendo watakayokuwa nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vkuhusu Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs) naishukuru na kuiomba Serikali kuzidi kuangalia vyuo hivi, kwani wanafunzi wanaomaliza katika vyuo hivi wataendelea kueneza elimu ya vitendo waliyoipata katika maeneo yao. Mheshimiwa Waziri nashauri mabweni yaendelee kujengwa na kuboreshwa katika vyuo hivi ili vyuo hivi watoto wengi waweze kudahiliwa. Namuomba Mheshimiwa Waziri jambo hili aliangalie na kulipa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia kwa kuongelea walimu wa masomo ya sayansi. Naomba mikakati iongezeke ya kupata walimu wengi wa sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.