Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na fursa ya kuwepo hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kasim Majaliwa pamoja na Mheshimiwa Jenista Mhagama, Mheshimiwa Abdallah Possi na Mheshimiwa Anthony Mavunde, wote kwa pamoja kwa kuunda timu ya uhakika ya kuleta maendeleo. Niipongeze pia timu ya wataalam wa ofisi zote chini ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nipongeze hotuba nzuri ambayo ilisomwa na Waziri Mkuu ambayo imegusa nyanja zote. Niipongeze Serikali kwa kuja na mpango wa kuelekea kwenye uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti,kwanza kabisa naomba niishauri Serikali na wataalam, ijipange kuangalia suala zima la sera na sheria pamoja na kanuni mbalimbali ili tufanikiwe katika mipango yetu ya kuwa na uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi naona kutakuwa na tatizo katika mfumo wetu wa gharama za juu kwenye uzalishaji. Viwanda vingi nchini vimeshindwa kupata mafanikio kwa sababu ya sera yetu ya kodi na tozo mbalimbali zinazotozwa na Taasisi za Udhibiti (Regulatory Bodies), ndiyo maana hata baada ya kuongeza kodi ya kusafirisha nje malighafi, mfano ngozi au korosho ghafi, lakini bado zinasafirishwa ghafi kutokana na gharama mbalimbali za tozo na kodi zinazotozwa katika usindikaji ndani ya nchi kuwa kubwa kuliko hiyo export levy.
Pia bidhaa nyingi huingizwa nchini bila kodi yoyote, kama mbegu, madawa ya kilimo (viuatilifu) na mifugo (dawa za chanjo na zinazozalishwa nchini kutozwa kodi na tozo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali iangalie namna ya kuondoa tozo hizo zinazotolewa na wadau kwa ajili ya huduma zao na badala yake Serikali igharamie gharama za uendeshaji wa taasisi hizo. Leo hii zimebaki kufanya kazi ya kukusanya tozo zaidi badala ya huduma. Baadhi ya tozo hizo ziondolewe kabisa kwa sababu zinaleta ushindani usio wa haki (no fair trade practice); waliosajiliwa hutoza zaidi kuliko wasiosajiliwa. Taasisi nyingine hufanya kazi zinazofanana. Pia Serikali iangalie namna ya kuondoa urasimu na kupunguza muda wa kutoa maamuzi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine muhimu ni kuongeza bajeti ya utafiti. Utafiti ndani ya nchi unatakiwa kuboreshwa sana. Njia pekee ni kuwekeza katika rasilimali watu, vifaa na kutoa taarifa za utafiti huo (dissemination of information).
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba tuishauri Serikali kama Bunge, itangaze bila kukosa mafanikio yote yaliyofanywa na Serikali. Serikali haitangazi yote yaliyofanywa kutoka miaka mingi iliyopita. Hii inatoa fursa kwa Wapinzani wa Serikali yetu kutusema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.