Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali, Wizara ya Elimu na viongozi wote wa Wizara ya Elimu kwa juhudi kubwa za kuendeleza elimu nchini kwa manufaa ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na waliopendekeza watoto wa kike wanapopata ujauzito wakiwa bado wanafunzi waruhusiwe kurejea shuleni baada ya kujifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya watu wazima iimarishwe zaidi ili kuwasaidia wale vijana walioacha shule mapema na waliokosa kwenda shule kwa sababu mbalimbali zikiwemo umaskini wa familia zao.


Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya ufundi ipewe nguvu na shule za ufundi zipatiwe vifaa vya kisasa ili wanafunzi wanapomaliza waweze kujiajiri, pia waweze kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja na nawatakia kazi njema.