Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa. Awali ya yote naunga mkono hoja na napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wa Fedha kwa bajeti nzuri na vilevile kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuirejeshea nchi yetu sifa na heshima yake ya zamani, sifa na heshima ya kuthubutu, sifa na heshima ya kupigania haki, usawa, na uhuru bila kigugumizi, bila uoga na bila hata kujali aliyeko upande wa pili, je, ana fedha nyingi, ni mkubwa sana au yukoje. Na msimamo huo dunia nzima ilitambua kwamba hiyo ndio Tanzania. Mwalimu alianza kuonesha sifa hii ya Tanzania mara tu baada ya uhuru baada ya kuiweka nchi yetu kama ngome kuu ya upiganiaji uhuru katika Bara la Afrika na dunia yote ilijua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikukumbushe kitu kimoja kwamba katika hali ya kawaida huwa ni tajiri tu ndiye anayeweza kumuwekea vikwazo mtu maskini, lakini kipindi cha Mwalimu nchi masikini ya Tanzania ilikuwa inawawekea vikwazo hata nchi kubwa. Na ukiwekewa vikwazo na Tanzania una hali mbaya, chukulia mfano Uingereza walipoanza kuchezacheza na haki ya uhuru wa watu wa Zimbabwe, tarehe 16 Disemba, 1965 Tanzania tukavunja uhusiano wa kidiplomasia na Uingereza na dunia ikaona, just a question of principle! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulipoungana na Zanzibar mwaka 1964 Ujerumani wakaanza kutumia ile wanaita the Hallstein Doctrine ambayo ilikuwa inasema kama wewe ni rafiki wa Ujerumani Magharibi basi vunja urafiki na Ujerumani Mashariki; Mwalimu akasema I see, hebu acheni kutuchezea hapa, ondokeni Wajerumani wote. Hiyo, ndiyo Tanzania, Tanzania ya kuthubutu, Tanzania yenye principles. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulifundishwa na Mwalimu kwamba Nchi hii ili iweze kuendelea hatuhitaji big brother, hatuhitaji pesa, hiyo ni akili ya kitumwa, pesa ni matokeo. Tunachohitaji ni vitu vinne tu; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, huo ndio ulikuwa msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mjadala wa makinikia au mashapo kwa mujibu wa Kamusi tuliyoizindua tu hapa jana; mjadala huu ambao umeendelea kwa wiki kama mbili hivi, hauakisi Tanzania ya Nyerere. Wakati wananchi wanaunga mkono na kushangilia uthubutu wa Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kutetea rasilimali za nchi na wao wanaelewa mikataba tuliyoingia, mchanga unachukuliwa yanaachwa mashimo hapa, hakuna hata makubaliano kwamba basi mkishachenjua kule turudishieni mchanga tuzibe haya mashimo au mtatengenezaje?

Mheshimiwa Spika, tuna makampuni hapa kama Williamson Diamond, miaka 77 haipati faida lakini ikiwa Botswana inapata faida, wananchi wanalielewa hilo, lakini sisi wasomi sasa tunasema hapana, jamani tuwe waangalifu, tuwe waangalifu sana! Oooh, wazungu hawa, tuwe waangalifu nao; mimi nashangaa.

Mheshimiwa Spika, sasa ili tuendelee tunahitaji vitu vinne watu, ardhi, siasa na uongozi bora, sasa hivi imebadilika imekuwa ili tuendelee tunahitaji fedha na wazungu, maana tunawaogopa wazungu kupita kiasi, imenitisha.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, leo hii tuna vita ya kiuchumi, kijana msomi, mwanasheria, unasimama hapa unatutishia nyau! Ooh! Tuna MIGA na Wanyakyusa kuna watu wanaitwa kina Minga, wananiuliza hivi huyu Minga ametokea wapi? Tuna MIGA! What is MIGA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mbunge wa Mwibara hapa, alituletea mkataba hapa, kasoma tu kifungu kimoja, Ibara ya 12, lakini namwambia asome na ya 11, hatuwezi kushindwa kesi chini ya sheria hii ndogo ya MIGA, ni mkataba wa kawaida tu kama mikataba mingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, taarifa ya Profesa Osoro, ya Mruma ni takataka! Huo ni umamluki wa hali ya juu. Tuko kwenye vita! Tuko kwenye vita hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sio tu MIGA, lakini sisi tuna mikataba ya kimataifa inayosimamia good faith katika mikataba. Tuna UN Convention on Contrast for International of Sale of Goods, tuna UCC ambayo ni Unfair Commercial Code ambayo tunaitumia, yote inasisitiza good faith katika mikataba. Good faith inatokea wapi, mikataba hii ya madini ambapo mtu anasema nachukua mchanga wako kwenda kuchenjua, tuna-calculate percentage kule, kumbe ameshauza siku nyingi. There is no good faith! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, MIGA Convention yenyewe inasema nini; MIGA inasema ukitaka kutumia MIGA faida yake hapa lazima uheshimu sheria za nchi. Sheria za nchi zinasema nini? Zinasema kwamba ukitaka kuingia mkataba lazima kuwepo na union of minds, wanasheria wanajua, tunaita concensus ad idem, haiwezekani ikawepo concensus wakati wewe unamwambia mwenzako naenda kuchenjua halafu nakokotoa, kumbe huwa kabla ya kuchimba umeshauza hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndio maana nasema hatuwezi hata kidogo kushindwa hiyo kesi. Tuliweza kushinda mtihani wa Devolution Agreements wakati wa uhuru, tutashindwa MIGA? Tutashindwa MIGA? Tukishindwa kesi hii basi tumezungukwa na Mayuda Iskariote wa kutisha, lakini nashukuru wako wachache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Devolution Agreements zilikuwa ni nini, niseme kwa kifupi. Tulipokuwa tunapata uhuru Barani Afrika Waingereza walikuwa wanakuja na mikataba inayosema, mimi nakubali mikataba yote aliyoingia Uingereza inayonibana inibane mimi kama nchi huru. Ni Mwalimu Nyerere peke yake aliyepeleka note ya kukataa hiyo Umoja wa Mataifa akisema mimi nilikuwa sijazaliwa kama taifa huru, mikataba hiyo mliingia kwa hiyari yenu hamkuni-consult, mlinitawala bila kibali changu, sitaki kuingia kwenye hiyo biashara; na tangu toka hapo ndipo ikazaliwa dhana katika Sheria ya Kimataifa inaitwa The Nyerere Doctrine of State Succession ambayo watu wengi wameifanyia mpaka Degree za Uzamivu, hii nchi ina historia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, msimamo wa Mwalimu uliokoa mengi sana nchi hii. Tulikuwa na Belbase Agreement alioingia Mwingereza na Ubelgiji. Mwingereza aliitoa Bandari ya Kigoma na Bandari ya Dar es Salaam kuwapa Wabelgiji waimiliki, tukakwepa kutokana na Mwalimu msimamo wake wa kwamba hatukubali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilishaunga mkono hoja.