Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nichangie hotuba iliyopo mbele yetu ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe masikitiko yangu kidogo au nitoe angalizo, nisamehewe kwa sababu nina mafua, nina flu kali kwa hiyo sauti yangu inawezekana isisikike vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais ni hotuba ambayo imekonga mioyo ya watu, ni hotuba ambayo mjadala wake ni wa kumsifia tu. Kwa nini nasema hivi? Hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati anaitoa hiyo tarehe 20 Novemba alichokuwa anakazia ni yale aliyoyafanya wakati wa kampeni yake. Kampeni yake imezunguka Tanzania nzima na kila eneo, yale aliyoyasema alikuja kuwasilisha kwenye Bunge ili Serikali yake iweze kuyafanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais kwa kuwa alikuwa anakerwa sana na umaskini wa nchi hii aliona ni afadhali ajionee mwenyewe yale ambayo alikuwa anayasikia. Kila eneo alilokwenda wamempa malalamiko yake ambayo Kata, Wilaya au Jimbo lile linahusika, kwa hiyo, ni pongezi kubwa sana kwake. Lakini si hilo tu hotuba yake haikuchagua imegusa makundi yote. Wakati anaunda Baraza lake la Mawaziri ametambua hilo akaunganisha Wizara ili ufanisi wa ahadi zake uwe karibu na wananchi, kwa hiyo, nampongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuchangia kwa kuokoa muda, nianze na huduma ya afya. Nimpongeze sana Naibu Waziri wa Afya, alikuja katika hospitali yetu ya Kitete, akajionea hali halisi lakini baada ya hapo aliweza kuchukua majukumu mengine na akaweza kutoa ahadi. Hospitali ya Kitete ambayo iko Mkoa wa Tabora ina changamoto nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya kwanza, hospitali ile inaitwa ya Hospitali ya Rufaa lakini hivi navyoongea hatuna madaktari bingwa. Inawezekana tatizo hilo ni la Mkoa wa Tabora lakini pia inawezekana ni nchi nzima. Tuna upungufu wa Madaktari Bingwa hususani upande wa gynecologist, akina mama wengi wanateseka lakini madaktari bingwa wa mifupa hawapo. Mimi niombe, kwa kuwa Hospitali ya Kitete ya Rufaa kwa wilaya zake saba ambazo ziko katika mkoa ule, niiombe Serikali itekeleze au angalau basi tuwe na madaktari ambao wanaweza wakawa na fani hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo katika hospitali ile tuna tatizo kubwa la mashine za kufulia nguo yaani laundry. Tatizo hilo linatokana na ongezeko la wagonjwa linalofanya ongezeko la nguo au mashuka kuwa kubwa. Mashine ile ina miaka zaidi ya 30. Hatujaletewa mashine ya kisasa ya kufulia nguo za wagonjwa, ukienda pale ni taabani. Ukiangalia mashuka hata upeleke leo, kesho halitakuwa katika hali nzuri. Kwa hiyo, naomba Serikali ya Chama cha Mapinduzi iangalie sekta hiyo ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna tatizo kubwa la madai ya wafanyakazi ingawa ni kidogo lakini ni mali yao. Niiombe Serikali, haya malimbikizo ya wafanyakazi inawavunja moyo ni lazima mtu alipwe kile ambacho amekifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vifaa tiba ni tatizo sana hasa kwa wodi ya akina mama. Kile kiwanda hakuna asiyekipitia hususani wanawake, ni kiwanda kigumu. Nashukuru Serikali angalau sasa hivi inapunguza vifo vya akina mama na watoto lakini huduma zingine bado zinalinganishwa na huduma za kawaida. Kwa hiyo, nashauri Serikali ya Chama cha Mapinduzi iangalie kwa jicho la huruma wodi za wanawake nchi nzima na hususani vijijini hakuna gloves, hakuna sindano, huyo mama unayemwambia gloves hazijui na wala maana yake pia haijui. Anachojua yeye ni kuongeza uzalishaji, tumeambiwa sisi tuongeze dunia. Kwa hiyo, niombe na nitoe angalizo kwa Wizara ya Afya iangalie ni jinsi gani inaweza kutusaidia kwa tatizo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, si hilo tu, nimpongeze Mheshimiwa Rais, kazi aliyofanya pale Muhimbili kupitia Kitengo cha MSD ni sifa kubwa, ni kazi nzuri, ameokoa mamilioni ya watu ambao wangekufa wasiokuwa na uwezo wa kwenda kununua dawa kwenye maduka ya watu binafsi. Kwa hiyo, niombe hospitali za Mikoa, Wilaya MSD wasogeze huduma pale ili angalau watu wa kawaida waweze kununua dawa kwa bei nafuu. Kwa hiyo, vifaa tiba, nadhani navyo viwe ni angalizo kwa kumsaidia Rais wetu kama mfano uliotolewa Muhimbili sasa hivi kila anayesimama pale anazungumzia habari hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ya shilingi milioni 50 kila kata au kila kijiji. Wakati wa mfuko wa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete wapo wajanja walichakachua wakafanya ile miradi kama ni yao wakafungua SACCOS zao. Ombi langu kwenye pesa hizi, ifuate na iangalie vikundi vya akina mama lishe, vikundi vya kilimo, vikundi vya walemavu, vikundi vya wajane na vikundi vya VICOBA. Kwa kufanya hivyo, fedha alizosema Mheshimiwa Rais shilingi milioni 50 watafaidika wananchi wengi, nchi hii ina wajanja wengi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ameelezea kuhusu ushuru mdogo mdogo, ni kero kwa akina mama, mtu anadaiwa Sh.200. Kwa hiyo, naomba hiyo nayo iwe angalizo kwa wale ambao watasimamia mfuko huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie habari ya barabara, ingawa Wabunge wote wa Tabora na mikoa mingine ya jirani wamezungumzia habari ya barabara. Barabara ya Chaya inaharibu utamu wa barabara yote na kazi zote zilizofanyika kutoka Itigi – Tabora, ni kilomita chache sana. Naomba Waziri mhusika atusaidie kwa hili. Tunazunguka tunahangaika, kilometa zinazozidi ni nyingi na walalahoi hawawezi kuzunguka kwa sababu bei inakuwa kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna barabara ya Urambo – Kaliua, ni kilometa 32 tu kuunganisha. Watu wanapata taabu kutoka Kigoma wakifika Kaliua wanatumia saa nyingi wanaichukia na Serikali yao. Kwa hiyo, naomba sana hilo liangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna barabara ya Sikonge. Naomba Waziri twende naye huko akaione barabara ya Sikonge inayokwenda Mpanda, kama atarudi amevaa hata koti, hawezi, wananchi wanateseka. Kwa hiyo, naomba barabara ya Tabora – Sikonge nayo ishughulikiwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna barabara nyingine ambayo inaunganisha Majimbo mawili, barabara ya Puge – Ndala – Simbo – Nkinga - Ziba ambayo inakwenda kwenye barabara kuu inayokwenda Singida, hii nayo ni kilometa chache. Naomba nayo waiweke katika mipango yao ili ikiwezekana twende pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kufufua viwanda, wamepewa miezi sita, kiwanda cha kwanza nchi hii kinachowadhulumu wananchi ni Kiwanda cha Nyuzi cha Tabora, ni mateso. Kiwanda kile Mbunge aliyepita Mheshimiwa Mzee Msigalo alitoa shilingi ndani ya Bunge hili.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, basi baada ya hapo, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais, mengine nitaandika kwa mkono, ahsante sana. (Makofi)