Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia katika Wizara ya Ulinzi. Kwanza nimpongeze Waziri wa Ulinzi, kaka yangu Mheshimiwa Hussein Mwinyi kwa kazi nzuri ambayo anaifanya katika kuliendesha Jeshi hili, nikupongeze sana kaka yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nigusie katika uchukuaji wa vijana kwenda JKT. Kwa upande wa Zanzibar uchukuaji wa vijana kwenda JKT tulikuwa tukilipigia kelele sana, nafikiri hata Bunge lililopita nimelizungumzia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wetu wa Zanzibar bado uchukuaji wa vijana hawa ni kidogo sana.

Kwa hiyo nimuombe sana Mheshimiwa Waziri, aweze kutusaidia kwa hili, aliangalie kwa macho mapana ili kuhakikisha vijana wetu kutoka Zanzibar wanaongezeka katika kuchukuliwa, na hasa kuangalia kwa sasa kama kauli yake juzi alivyoisema kwa makini kuwa vikosi vyote vya ulinzi, hata Jeshi la Polisi, basi watakuwa wanachukua vijana hawa kutoka ndani ya JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri aweze kutuongezea kwa upande wa Zanzibar kuchukua vijana hawa wa kwenda JKT angalau tufike vijana 600 kutoka vijana 300 ambao wapo sasa hivi. Nimuombe sana Mheshimiwa Waziri kwa hili aliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mheshimiwa Waziri nikuombe sana, nilikuwa nikilizungumza sana Zanzibar tuna Kikosi chetu cha JKU ambacho kinafanana sana na Kikosi hiki cha JKT, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri katika mipango yako na mazungumzo yako vijana hawa wa JKT ukitaka kuwachukua kwa kutoka upande wa Zanzibar ni bora sana kuchukua eneo hili la JKU kwa sababu unapata vijana ambao wanakuwa wameshapata mafunzo mazuri, vijana ambao wana mwelekeo mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri uweze kulifikiria hili. Mheshimiwa Waziri hili hata bajeti iliyopita mimi nililizungumzia sana kuhakikisha kama vijana unapotaka kuchukua basi uelekee katika kikosi hiki cha JKU kwa sababu, hiki kikosi tayari kuna vijana wameshaandaliwa kwa muda mrefu, vijana wazuri ambao wana haki ya kupelekwa katika JKT na kupata ajira ya jeshi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nigusie upandishaji wa vyeo vyeo vya juu kwa askari kutoka Zanzibar. Ni jambo la kushangaza sana kwamba hata hawa askari wetu kutoka Zanzibar bado upandishaji wao wa vyeo vya juu umekuwa hafifu sana katika jeshi hili. Kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri aweze kuliangalia hili kwa makini, hata akija akatoa maelezo yake hapo atueleze kuna askari wa vyeo vya juu wangapi kutika Zanzibar, kwa sababu tuangalie katika uwiano mzuri, ili tuweze kufika pazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu nigusie ile pension ya askari wastaafu wa zamani. Hili ni jambo kubwa sana Mheshimiwa Waziri, hawa wazee wanapostaafu huko wanalalamika sana. Kuna Sajenti aliyestaafu, sasa hivi pensheni yake analipwa takriban zaidi ya shilingi 600,000, lakini jambo la kushangaza sana yule yule Sajenti wa zamani ambaye ameondoka katika hili Jeshi hata nusu yake hafiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana hawa ni wazee wetu ambao wamefanyakazi kwa nguvu zao katika Jeshi hili lakini hatimaye basi malipo yao ni madogo sana.Wanapata taabu na wanaadhirika sana. Nimuombe Mheshimiwa Waziri aweze kuliangalia kwa makini suala hili ili kuhakikisha kwamba hawa wazee wetu wanapandishwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.