Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

HE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia hoja hii muhimu ya ulinzi wa nchi yetu na mipaka yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumshukuru Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Serikali yake hasa Waziri wa Ulinzi na wataalam wake kufika katika Jimbo langu la Morogoro Kusini Mashariki katika Wilaya ya Morogoro Vijijini kufuatilia uwanja wa ndege wa Jeshi letu pale Kizuka Ngerengere. Tunasema ahsante sana.

Mheshmiwa Mwenyekiti, pia namshukuru Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufulu kwa maamuzi yake ya kuagiza kutujengea barabara ya lami kutoka Ubena – Zomozi – Kizuka mpaka Ngerengere kupitia uwanja wa Kizuka.

Mheshiwa Mwenyekiti, baada ya shukrani hizo za watu wa Morogoro Kusini Mashariki hususani wananchi wa Tarafa ya Ngerengere na Tarafa ya Mvuha, naomba sasa nitoe ombi langu rasmi kwa Serikali hasa kwa Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tuna Kambi mbili za Jeshi pale Ngerengere yaani ya Kizuka na Sangasanga na kwa kuwa barabara itakayowekwa lami ni ya Ubena – Zomozi – Kizuka - Ngerengere na kwa kuwa umbali kutoka Kizuka - Ngerengere - Sangasanga siyo mbali na Kambi ya Sangasanga wanatumia barabara ya Mdaula – Sangasanga yenye urefu wa kilometa 10, kwa hiyo basi, naomba barabara hii nayo iwekwe lami kwani watoto hawa wa Sangasanga na Kizuka ni baba na mama mmoja ili wale Sangasanga wasione wametengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yangu kulipa uzito suala hili na hasa kwa umuhimu wa jeshi letu na hasa kikosi hiki cha Sangasanga kutokana na uzito wa majukumu yake. Naomba barabara ya Mdaula – Sangasanga - Ngerengere kuwekwa lami ili kuunganika na ile ya Ubena - Kizuka - Ngerengere na kurahisisha usafiri kwa jeshi letu na wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.