Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Sehemu kubwa ya mpaka kati ya Tanzania na Uganda iko Wilaya ya Misenyi – Kagera. Kama unavyofahamu kuna mambo mengi yanayoendelea katika mpaka huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iwe karibu zaidi na ifuatilie kila siku yanayoendelea kwenye mpaka huo kwa nia ya kuimarisha ulinzi, ujirani mwema na kuimarisha utangamano. Aidha, suala la ng’ombe wanaoletwa kutoka nchi jirani (Uganda) na kuja kula majani Tanzania inabidi liangaliwe kwa umakini na lidhibitiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwongozo uwe kwamba ardhi ya Tanzania itumiwe na Watanzania tu na kwamba wanaoleta mifugo kutoka nchi jirani wadhibitiwe na watumie ardhi ya nchi zao. Jambo hili la kudhibiti mifugo kutoka nchi jirani litawezekana tu kama wale tunaowapa majukumu ya kulinda mipaka wakizingatia miongozo wanayopewa na kuzingatia maadili ya Tanzania. Aidha, usalama wa Watanzania wanaoishi maeneo ya mipakani na mali zao upewe kipaumbele pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.