Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hii muhimu kwa nchi yetu. Kama ilivyo katika dira ya Taifa ya kulinda na kudumisha amani na usalama wa Taifa letu; pamoja kuendelea kulinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya maadui wa ndani na nje ya nchi yetu; usalama wa mipaka ya nchi, mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya nchi ya Tanzania na Malawi umekuwa wa muda mrefu hivyo kuendelea kuathiri ukuaji wa uchumi kwa nchi yetu hasa kwa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huo unaendelea kuathiri shughuli za uwekezaji katika eneo la Ziwa Nyasa na hivyo kufanya mdororo wa kiuchumi kwa wananchi na kupoteza mapato katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha aniambie mgogoro huu umefikia wapi ili kuweka mahusiano mazuri kati ya nchi ya Tanzania na Malawi na pia kuinua uchumi wa nchi yetu kupitia fursa zilizopo katika Ziwa Nyasa na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira kwa vijana waliopata mafunzo ya JKT; kumekuwa na changamoto kubwa ya ajira nchini na hii ni pamoja na vijana wanaomaliza mafunzo JKT na kupelekea vijana hawa kujiingiza katika vitendo vya uvunjaji wa amani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya nyuma taasisi za Kiserikali, kwa mfano TANAPA ilikuwa ikichukua vijana wengi waliomaliza JKT na kuwapatia ajira hali ambayo kwa sasa imepungua na kufanya nidhamu kupungua sana kwa taasisi zinazojihusisha na masuala ya ulinzi na usalama wa maliasili zetu.